Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • kr sura 17 uku. 182-191
  • Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi
  • Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Kama Vile Baba Alivyonifundisha, Ndivyo Ninavyosema”
  • Wahubiri Wanazoezwa ili Kuwa Waeneza-Injili
  • Ndugu Wanazoezwa ili Kutimiza Migao ya Pekee
  • Masomo Mbalimbali Yanayoongozwa na Tengenezo la Mungu Yanaonyesha Upendo wa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Je, Unafaidika Kabisa na Mafundisho Yanayotolewa na Yehova?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Ni Masomo Gani Yenye Kutayarishwa kwa Ajili ya Mapainia?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Shule ya Mazoezi ya Kihuduma—Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Ona Habari Zaidi
Ufalme wa Mungu Unatawala!
kr sura 17 uku. 182-191

SURA 17

Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Namna masomo mbalimbali ya kiteokrasi imetayarisha wahubiri wa Ufalme kutimiza migao yao

1-3. Yesu alichukua mipango gani ili kazi ya kuhubiri ifike mahali pote, na tunaweza kujiuliza maulizo gani?

YESU alihubiri katika muji wote wa Galilaya kwa muda wa miaka mbili. (Soma Mathayo 9:35-38.) Alitembelea miji na vijiji mbalimbali ili kufundisha katika masinagogi na kuhubiri kuhusu habari njema ya Ufalme. Kila mahali ambako alikuwa anahubiri, watu wengi sana walikuja kumusikiliza. Ndio sababu Yesu alisema kwamba “mavuno ni mengi,” na kwamba kuna lazima ya wafanyakazi wengi.

2 Yesu alichukua mipango ili kazi ya kuhubiri ifike kila mahali. Alifanya hivyo namna gani? Aliwatuma mitume wake 12 ili “kuhubiri ufalme wa Mungu.” (Lu. 9:1, 2) Inawezekana mitume walijiuliza namna gani wangeweza kutimiza kazi hiyo. Mbele ya kuwatuma, kwa upendo Yesu aliwapatia jambo fulani ambalo baba yake alikuwa amemupatia, ni kusema, aliwapatia mazoezi.

3 Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza: Yesu alipata mazoezi gani kutoka kwa Baba yake? Yesu aliwapatia mitume wake mazoezi gani? Tuseme nini kuhusu wafuasi wa Masiya Mufalme leo, amewapa mazoezi ili kutimiza kazi yao? Ikiwa jibu ni ndiyo, amefanya hivyo namna gani?

“Kama Vile Baba Alivyonifundisha, Ndivyo Ninavyosema”

4. Ni wapi na ni wakati gani Yesu alifundishwa na Baba yake?

4 Yesu alionyesha waziwazi kwamba alifundishwa na Baba yake. Wakati alikuwa anahubiri, Yesu alisema hivi: “Kama vile Baba alivyonifundisha, ndivyo ninavyosema.” (Yoh. 8:28) Ni wapi na ni wakati gani Yesu alifundishwa? Ni wazi kwamba, Yesu alianza kufundishwa na Mungu kisha tu kuumbwa. (Kol. 1:15) Kwa sababu Mwana huyo muzaliwa wa kwanza wa Mungu alikuwa pembeni ya Baba yake huko mbinguni, alikuwa na miaka mingi sana ya kumusikiliza na kumutazama ‘Mufundishaji [huyo] Mukubwa.’ (Isa. 30:20) Kwa hiyo, Yesu alijifunza mengi juu ya sifa, kazi, na makusudi ya Baba yake.

5. Ni nini Baba alimufundisha mwana wake kuhusu kazi ambayo angetimiza hapa duniani?

5 Kwa wakati uliofaa, Yehova alimufundisha Mwana wake kuhusu kazi ambayo angetimiza hapa duniani. Acha tuchunguze unabii ambao unaonyesha uhusiano ambao Mufundishaji Mukubwa alikuwa nao pamoja na Mwana wake muzaliwa wa kwanza. (Soma Isaya 50:4, 5.) Unabii huo unasema kwamba Yehova alikuwa anamuamusha Mwana wake “asubuhi baada ya asubuhi.” Maneno hayo ya mufano, yanatusaidia kufikiria mwalimu ambaye anamuamusha mwanafunzi wake asubuhi sana ili kumufundisha. Kitabu kimoja ambacho kinafasiria Biblia kinasema hivi: “Ni kama vile Yehova . . . anamupeleka kwenye masomo, kama vile wanamupeleka mwanafunzi kwenye masomo, na anamufundisha namna ya kuhubiri na pia mambo ya kuhubiri.” Kwenye “masomo” hayo ya mbinguni Yehova alimufundisha Mwana wake “jambo la kutangaza na la kusema.” (Yoh. 12:49) Pia, Yehova alimupatia Mwana wake mazoezi kuhusu namna ya kufundisha.a Wakati Yesu alikuwa hapa duniani, alitumia vizuri mazoezi ambayo alipewa kwa kutimiza kazi yake ya kuhubiri. Lakini pia, alitumia mazoezi hayo kwa kuwazoeza wanafunzi wake watimize kazi yao.

6, 7. (a) Yesu aliwapatia mitume wake mazoezi gani, na mazoezi hayo yaliwasaidia kufanya nini? (b) Yesu amehakikisha kwamba wafuasi wake hapa duniani wapewe mazoezi gani?

6 Kama vile imeonyeshwa mwanzoni mwa sura hii, ni mazoezi gani Yesu aliwapatia mitume wake? Kulingana na Mathayo sura ya 10, Yesu aliwapatia maagizo kuhusu kazi ya kuhubiri, kama vile: mahali pa kuhubiri (mustari wa 5, na wa 6), habari ya kuhubiri (mustari wa 7), ulazima wa kumutegemea Yehova (mustari wa 9, na wa 10), namna ya kuanza mazungumuzo na watu (mustari wa 11-13, namna wangefanya ikiwa watu wanakataa kuwasikiliza (mustari wa 14, na wa 15), na namna ya kufanya ikiwa wanateswa kwa sababu ya imani yao (mustari wa 16-23).b Maagizo hayo yenye kuwa wazi ambayo Yesu aliwapatia mitume wake, yaliwasaidia kuwa kwenye mustari wa mbele ao kuongoza kazi ya kuhubiri habari njema wakati wao.

7 Tuseme nini juu ya siku zetu? Yesu ambaye ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu amepatia wafuasi wake kazi ya lazima sana kuliko zote, ni kazi ya kuhubiri ‘hii habari njema ya Ufalme katika dunia yote inayoikaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.’ (Mt. 24:14) Mufalme, ametuzoeza ili tutimize kazi hii ya lazima sana kuliko zote? Bila shaka, ndiyo! Mufalme iko mbinguni; kutoka huko anahakikisha kwamba wafuasi wake wanapokea mazoezi kuhusu namna ya kuhubiri inje ya kutaniko na pia kuhusu namna ya kutimiza migao ya pekee katika kutaniko.

Wahubiri Wanazoezwa ili Kuwa Waeneza-Injili

8, 9. (a) Ni nini kusudi kubwa la Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi? (b) Namna gani Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi yamekusaidia uwe na matokeo mazuri katika kazi yako ya kuhubiri?

8 Kwa miaka mingi, tengenezo la Yehova limetumia mikusanyiko, na mikutano ya kutaniko, kama vile Mukutano wa Utumishi ili kuzoeza watu wa Mungu kwa ajili ya kazi ya kuhubiri. Hata hivyo, kuanzia miaka ya 1940, ndugu ambao walikuwa wanaongoza kwenye makao makubwa walianza mipango ya kuzoeza watu wa Mungu kupitia masomo mbalimbali.

9 Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Kama vile tulijifunza katika sura ambayo ilitangulia, masomo hayo yalianza kuongozwa katika mwaka wa 1943. Kusudi la masomo hayo, ilikuwa nikuzoeza tu wanafunzi ili watoe hotuba nzuri kwenye mikutano ya kutaniko? Hapana. Tangu mwanzo, kusudi kubwa la masomo ilikuwa ni kuzoeza watu wa Mungu watumie zawadi yao ya kusema ili kumusifu Yehova katika mahubiri. (Zab. 150:6) Masomo hayo yaliwasaidia ndugu na dada wote ambao walijiandikisha kuwa wahubiri wa Ufalme wenye matokeo zaidi. Sasa mazoezi kama hayo yanatolewa kupitia mukutano wa katikati ya juma.

10, 11. Leo, ni nani anaweza kujiandikisha kwenye Masomo ya Gileadi, na masomo hayo yana kusudi gani?

10 Masomo ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower. Masomo ambayo yanajulikana leo kwa jina la Masomo ya Biblia ya Gileadi, yalianza Siku ya Kwanza tarehe 1 Mwezi 2, 1943. Mwanzoni masomo hayo yalianzishwa ili kuzoeza mapainia na watumishi wengine wa wakati wote ili waweze kufanya kazi ya umisionere kila mahali ambapo kuna lazima ya wahubiri duniani pote. Lakini kuanzia Mwezi wa 10, 2011, maagizo mapya yalitolewa ambayo yalionyesha kwamba, ni wale tu ambao wako tayari katika utumishi wa wakati wote ndio wanakubaliwa, ni kusema, mapainia wa pekee, waangalizi wenye kusafiri na wake zao, Wanabeteli, na wamisionere wengine ambao walikuwa hawajahuzuria masomo hayo.

11 Mazoezi ambayo yanatolewa kwenye Masomo ya Gileadi yana kusudi gani? Mwalimu mumoja ambaye amekuwa mwalimu kwa miaka mingi kwenye masomo hayo, anajibu hivi: “Kusudi la masomo hayo ni kutia nguvu imani ya wanafunzi kwa kujifunza sana Neno la Mungu na kuwasaidia wawe na sifa za kiroho ambazo wanahitaji ili kupambana na matatizo mbalimbali ambayo watakutana nayo katika migao yao. Pia, kusudi kubwa ni kuwafanya wanafunzi wawe na tamaa zaidi ya kufanya kazi ya kueneza injili.”—Efe. 4:11.

12, 13. Masomo ya Gileadi yamekuwa na matokeo gani mazuri juu ya kazi ya kuhubiri ya duniani pote? Toa mufano.

12 Masomo ya Gileadi yamekuwa na matokeo gani juu ya kazi ya kuhubiri ya duniani pote? Kuanzia mwaka wa 1943, ndugu na dada zaidi ya 8500 wamepata mazoezi kwenye masomo hayo,c na wamisionere hao wemetumikia katika inchi zaidi ya 170 duniani. Wamisionere wametumia vizuri mazoezi ambayo wamepata kwa kufanya kazi ya kuhubiri kwa bidii na pia kwa kuzoeza wengine wafanye hivyo. Mara nyingi, wamisionere waliongoza kazi ya kuhubiri katika maeneo ambayo yalikuwa na wahubiri wadogo ao maeneo ambayo hayakuwa hata na muhubiri mumoja wa Ufalme.

13 Fikiria jambo ambalo lilitokea katika inchi ya Japani, ambako kazi ya kuhubiri ilikuwa kama yenye kusimamishwa wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Katika Mwezi wa 8, 1949, kulikuwa karibu wahubiri kumi katika inchi ya Japani. Lakini mwisho wa mwaka huo, wamisionere 13 ambao walipata mazoezi kwenye Gileadi walikuwa wanahubiri kwa bidii katika inchi ya Japani. Kisha, wamisionere wengine zaidi walitumwa katika inchi hiyo. Kwanza, walijikaza sana ili kuhubiri katika miji mikubwa-mikubwa; kisha wakaenda katika miji ingine. Wamisionere hao walitia moyo wanafunzi wao wa Biblia na pia wahubiri wengine kufanya kazi ya upainia. Bila shaka, bidii ambayo wamisionere hao walionyesha ilileta matokeo mazuri. Leo, kuna wahubiri wa Ufalme zaidi ya 216000 katika inchi ya Japani, na wahubiri karibu 40 juu ya 100 ni mapainia!d

14. Masomo mbalimbali ya kiteokrasi yanatoa ushuhuda gani wenye nguvu? (Soma pia kisanduku “Masomo Mbalimbali Ambayo Yanazoeza Wahubiri wa Ufalme,” ukurasa wa188.)

14 Masomo mengine ya kiteokrasi. Masomo ya Mapainia, Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Bibi zao, na Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi, yamesaidia ndugu na dada ambao wamealikwa kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova, na pia kuwa mufano muzuri katika kazi ya kueneza injili kwa bidii.e Masomo hayo yote ya kiteokrasi ni ushuhuda wenye nguvu kwamba Mufalme amezoeza wafuasi wake kutimiza kazi yao.​—2 Tim. 4:5.

Ndugu Wanazoezwa ili Kutimiza Migao ya Pekee

15. Ndugu walio na madaraka katika tengenezo wanapenda kumuiga Yesu namna gani?

15 Tukumbuke tena unabii wa Isaya ambao unasema kwamba Yesu anafundishwa na Mungu. Kwenye “masomo” hayo ya mbinguni, Mwana alijifunza namna ya kumujibu yeye aliyechoka kwa neno linalofaa. (Isa. 50:4) Yesu alitumikisha mafundisho hayo; wakati alikuwa hapa duniani, aliwapatia kitulizo wale ‘waliotaabika na kulemewa na mizigo.’ (Mt. 11:28-30) Kwa kuiga mufano wa Yesu, wanaume ambao wana madaraka fulani wanapenda kuwa watu ambao wanatolea ndugu na dada zao kitulizo. Ndio sababu masomo mbalimbali yemeanzishwa ili kusaidia ndugu wenye kustahili wapate matokeo mazuri wakati wanawatumikia ndugu na dada.

16, 17. Masomo ya Huduma ya Ufalme yana kusudi gani? (Soma pia maelezo mengine.)

16 Masomo ya Huduma ya Ufalme. Masomo hayo yalianzishwa tarehe 9 Mwezi wa 3, 1959, katika muji wa South Lansing, New York. Waangalizi wenye kusafiri na watumishi wa kutaniko (leo waratibu wa baraza la wazee) walialikwa ili kuhuzuria masomo hayo kwa muda wa mwezi moja. Kisha, habari ambazo walijifunza kwenye masomo hayo zilitafsiriwa katika luga zingine, na hatua kwa hatua ndugu wengine katika dunia yote walianza kupewa mazoezi kwenye masomo hayo.f

Ndugu Lloyd Barry anafundisha kwenye Masomo ya Huduma ya Ufalme katika inchi ya Japani, mwaka wa 1970

17 Kuhusu kusudi la Masomo ya Huduma ya Ufalme, Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1962 kilisema hivi: “Katika ulimwengu huu ambao watu wana mambo mengi ya kufanya, mwangalizi katika kutaniko la Mashahidi wa Yehova anapaswa kuwa mwanaume ambaye anaweza kupanga maisha yake vizuri. Jambo hilo linaweza kumusaidia akazie uangalifu zaidi ndugu na dada wote katika kutaniko, na pia kumufanya awe baraka kwa kutaniko lote. Hapaswe kusahau familia yake kwa sababu ya kuhangaikia kutaniko, kwa hiyo, anapaswa kutumia akili nzuri. Bila shaka, watumishi wa makutaniko katika dunia yote wamepewa pendeleo kubwa sana la kuhuzuria Masomo ya Huduma ya Ufalme ili wapewe mazoezi ambayo yatawasaidia kufanya yote ambayo Biblia inasema mwangalizi anapaswa kufanya!”​—1 Tim. 3:1-7; Tito 1:5-9.

18. Watu wote wa Mungu wanafaidika na Masomo ya Huduma ya Ufalme namna gani?

18 Watu wote wa Mungu wamefaidika na Masomo ya Huduma ya Ufalme. Namna gani? Wakati wazee na watumishi wa huduma wanatumia mambo ambayo wamefundishwa kwenye masomo hayo, kama Yesu, wanakuwa chanzo cha kitulizo kwa ndugu na dada zao katika makutaniko. Haufurahie wakati wazee ao watumishi wa huduma wanatumia maneno ya upole, wakati wanakusikiliza kwa uangalifu ao wakati wanakutembelea ili kukutia moyo? (1 Tes. 5:11) Wanaume hao wenye kustahili ni baraka kubwa kwa makutaniko!

19. Ni masomo gani mengine ambayo Halmashauri ya Ufundishaji inasimamia, na masomo hayo yote yana kusudi gani?

19 Masomo mengine ya kiteokrasi. Halmashauri ya Ufundishaji ya Baraza Lenye Kuongoza inasimamia masomo mengine ambayo yanapatia mazoezi ndugu walio na madaraka katika tengenezo. Masomo hayo yote yana kusudi la kusaidia ndugu wenye madaraka, kama vile wazee wa kutaniko, waangalizi wenye kusafiri, na ndugu wa Halmashauri ya Tawi ili waweze kutimiza kazi yao vizuri. Mazoezi hayo ambayo yanategemea Biblia yanawatia ndugu hao moyo waendelee kulinda hali yao nzuri ya kiroho wakati wanasaidia kondoo za Yehova ambao amewapatia wachunge.​—1 Pet. 5:1-3.

Masomo ya Mazoezi ya Kihuduma ambayo yalifanywa kwa mara ya kwanza katika inchi ya Malawi, mwaka wa 2007

20. Sababu gani Yesu alisema kweli wakati alisema kwamba sisi wote ‘tunafundishwa na Yehova,’ na umeazimia kufanya nini?

20 Ni wazi kwamba Masiya-Mufalme amehakikisha kwamba wafuasi wake wanazoezwa vizuri. Mazoezi hayo yote yametoka juu mbinguni: Yehova alimuzoeza Mwana wake, na Mwana wake anawazoeza wanafunzi wake. Kwa hiyo, alisema kweli wakati alisema kwamba sisi wote ‘tunafundishwa na Yehova.’ (Yoh. 6:45; Isa. 54:13) Acheni tuazimie kupata faida kabisa ya mafundisho yote ambayo Mufalme ametupatia. Pia acheni tukumbuke kwamba kusudi kubwa la mazoezi yote ambayo tunapewa ni kutusaidia tuendelee kuwa wenye nguvu kiroho ili tuweze kutimiza kazi yetu kwa ukamilifu.

a Tunajua namna gani kwamba Baba alimufundisha Mwana wake namna ya kufundisha? Fikiria jambo hili: Yesu alitumia mifano mingi katika mafundisho yake ili kutimiza unabii ambao uliandikwa miaka mingi mbele ya kuzaliwa kwake. (Zab. 78:2; Mt. 13:34, 35) Kwa kweli, Yehova ambaye aliandikisha unabii huo, alijua vizuri mbele ya wakati kwamba Mwana wake atatumia mifano katika mafundisho yake.​—2 Tim. 3:16, 17.

b Kisha miezi fulani, Yesu ‘akachagua wengine 70 na akawatuma wawili-wawili’ katika mahubiri. Aliwapatia pia mazoezi.​—Lu. 10:1-16.

c Wamisionere fulani walihuzuria Masomo ya Gileadi zaidi ya mara moja.

d Ili kujua zaidi juu ya kazi ambayo imetimizwa duniani na wamisionere ambao wamezoezwa kwenye Gileadi, soma sura ya 23 ya kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu.

e Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Bibi zao, na Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi, yamechangwa pamoja na sasa yanaitwa Masomo kwa Ajili ya Waeneza Injili wa Ufalme.

f Leo, wazee wote wanafaidika na Masomo ya Huduma ya Ufalme. Muda wa masomo hayo unabadilika kila mara, na masomo hayo yanafanywa kisha miaka fulani. Kuanzia mwaka wa 1984, watumishi wa huduma wamepewa pia mazoezi kupitia masomo hayo.

Ufalme Ni Jambo la Kweli

  • Ni mazoezi gani Yesu alipewa na Baba yake?

  • Namna gani Mufalme amezoeza wafuasi wake ili wawe waeneza-injili?

  • Namna gani ndugu wenye kustahili wamezoezwa ili kutimiza madaraka yao?

  • Unaweza kuonyesha namna gani kwamba unafurahia mazoezi ambayo Mufalme ametolea wafuasi wake?

MASOMO MBALIMBALI AMBAYO YANAZOEZA WAHUBIRI WA UFALME

UTUMISHI NA MAISHA YA MUKRISTO

Kusudi: Kuzoeza ndugu na dada ili wawe wahubiri na walimu wa habari njema wenye matokeo.

Muda: Mazoezi ya kuendelea.

Mahali: Jumba la Ufalme.

Kujiandikisha: Mukutano wa katikati ya juma unatufundisha kujua namna ya kutafuta habari na kuitoa katika njia yenye kufundisha. Pia, tunajifunza jinsi ya kusikiliza wengine na kufikiria mahitaji yao ya kiroho, kuliko kufikiria mahitaji yetu tu.”

Faida: Mukutano wa katikati ya juma unatufundisha kujua namna ya kutafuta habari na kuitoa katika njia yenye kufundisha. Pia, tunajifunza jinsi ya kusikiliza wengine na kufikiria mahitaji yao ya kiroho, kuliko kufikiria mahitaji yetu tu.”

Arnie, ambaye ni mwangalizi mwenye kusafiri kwa miaka mingi, anasema hivi: “Nilikuwa mwenye kugugumiza na ilikuwa vigumu kwangu kuwatazama watu wakati ninazungumuza nao. [Mukutano] huu umenisaidia kuwa na uhakika. Pia Yehova amenisaidia kwa sababu mazoezi ambayo nimepata kwenye mukutano huu yamenisaidia nijue ufundi wa kupumua vizuri na wa kukazia akili mambo ambayo ninazungumuzia. Ninafurahi sana kwa sababu nimepata uwezo wa kumusifu Mungu katika kutaniko na katika mahubiri.”

MASOMO KWA AJILI YA WAZEE WA KUTANIKOg

Kusudi: Ni kusaidia wazee wakuwe na hali muzuri zaidi ya kiroho na watimize vizuri madaraka yao katika kutaniko.

Muda: Siku tano.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; mara nyingi yanafanywa kwenye Majumba ya Ufalme ya karibu ao kwenye Jumba la Mikusanyiko.

Kujiandikisha: Biro ya tawi inaalika wazee.

Faida: Ona maelezo fulani ya ndugu ambao walisoma darasa la 92 la masomo hayo katika muji wa Patterson, New York, Amerika (États-Unis):

“Masomo hayo yameniletea faida nyingi, yamenisaidia nijichunguze na kuona namna ninaweza kuhangaikia kondoo wa Yehova.”

“Nitatumikisha mazoezi yote ambayo nilipata katika maisha yangu yote.”

MASOMO YA MAPAINIA

Kusudi: Kusaidia mapainia ‘watimize kwa ukamili’ huduma yao.​—2 Tim. 4:5.

Muda: Siku sita.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; mara nyingi yanafanywa kwenye Jumba la Ufalme la karibu.

Kujiandikisha: Wale ambao wako mapainia kwa muda wa mwaka moja wanaandikwa moja kwa moja na mwangalizi wao wa muzunguko na wanajulishwa kwamba watasoma. Mapainia fulani wa zamani ambao hawakusoma katika miaka tano ambayo imepita wanaweza kualikwa.

Faida: Dada Lily anasema hivi: “Masomo yamenisaidia kupambana na magumu ambayo ninapata katika mahubiri na katika maisha yangu. Namna yangu ya kujifunza, kufundisha na kutumia Biblia imekuwa muzuri zaidi. Nimetayarishwa vizuri ili kuwasaidia wengine, kuunga mukono wazee, na kusaidia ili kuwe na maendeleo katika kutaniko.”

Brenda, ambaye amehuzuria masomo mara mbili, anasema hivi: “Masomo hayo yamenisaidia sana kuhangaikia zaidi mambo ya kiroho, kuzoeza zamiri yangu, na kutumia uwezo wangu ili kusaidia wengine. Bila shaka Yehova si muchoyo!”

MASOMO YA WANABETELI WAPYA

Kusudi: Masomo hayo yametayarishwa ili kuwasaidia wanabeteli wapya watimize vizuri utumishi wao kwenye Beteli.

Muda: Siku ine kwa saa ine kila siku.

Mahali: Beteli.

Kujiandikisha: Wanabeteli wenye kudumu ao Wafanyakazi wenye kujitolea ambao wanatumika kwenye Beteli kwa muda fulani (mwaka moja ao zaidi) wanaandikishwa moja kwa moja.

Faida: Ndugu Demetrius, ambaye alihuzuria masomo hayo katika miaka ya 1980, anasema hivi: “Masomo hayo yalinisaidia kutengeneza mazoea yangu ya kujifunza Biblia na yalinitayarisha ili niweze kupitisha miaka mingi kwenye Beteli. Walimu, mazoezi ambayo nilipata, na mashauri mazuri ambayo nilipewa yalinihakikishia kwamba Yehova ananihangaikia kwa upendo na anapenda nipate matokeo mazuri katika utumishi wangu wa Beteli.”

MASOMO KWA AJIILI YA WAENEZA-INJILI WA UFALMEh

Kusudi: Kupatia mazoezi ya pekee wale walio katika utumishi wa wakati wote (bibi na bwana, ndugu wasio na bibi, na dada ambao hawajaolewa) ili waweze kumutumikia Yehova zaidi na kutumiwa zaidi na tengenezo lake. Wengi ambao watasoma kwenye masomo hayo watatumwa katika maeneo ya inchi ambako kuna lazima kubwa. Wanafunzi walio chini ya miaka 50 wanaweza kutumikia kwa muda kama mapainia wa pekee ili waweze kufungua maeneo mapya ambayo hayajahubiriwa ili kueneza injili huko.

Muda: Miezi mbili.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi; mara nyingi yanafanywa kwenye Jumba la Ufalme ao kwenye Jumba la Mikusanyiko.

A sister in the ministry

Ndugu na dada wanapata faida ya mazoezi ya kiteokrasi

Kujiandikisha: Wale ambao wanaalikwa ni ndugu na dada wenye kuwa katika utumishi wa wakati wote, na walio na miaka kati ya 23 na 65. Wanapaswa kuwa na afya nzuri na uwezo wa kutumikia katika eneo lolote ambalo kuna lazima kubwa. Tena wanapaswa kuwa na roho hii: “Mimi hapa! Nitume mimi!” (Isa. 6:8) Wote ambao wanaalikwa kwenye masomo hayo (ndugu wasio na bibi, ao dada wasioolewa, na pia bibi na bwana) wanapaswa kuwa wamefanya kazi ya upainia kwa miaka mbili hivi bila kuacha. Bibi na bwana wanapaswa kuwa wameoana kumepita miaka mbili hivi. Kila ndugu anapaswa kuwa muzee ao mutumishi wa huduma kwa muda wa miaka mbili hivi yenye kufuatana ili astahili kualikwa. Ikiwa masomo haya yanafanywa katika inchi yenu, mukutano utafanywa kwenye mukusanyiko wa eneo ili kuwatolea habari zaidi wale ambao wanapenda kuhuzuria masomo hayo.

Faida: Wale ambao walialikwa kwenye Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Bibi na Masomo kwa Ajili ya Ndugu na Bibi Zao wameonyesha kwamba wamepata faida nyingi. Katika mwaka wa 2013, Baraza Lenye Kuongoza Iiliamua kuchanga masomo hayo mawili. Yanaitwa sasa Masomo kwa Ajili ya Waeneza Injili wa Ufalme. Sasa mapainia wengi na hata dada wasioolewa, wataweza kufaidika na masomo hayo.

MASOMO YA BIBLIA YA GILEADI YA WATCHTOWER

Kusudi: Wale ambao wamezoezwa kwenye masomo hayo wanaweza kuwa waangalizi wenye kusafiri, wamisionere katika maeneo fulani, ao kuwa Wanabeteli. Wakati wanatumia mazoezi ambayo wamepata wanasaidia kufanya kazi ya kuhubiri na ya Beteli iwe nguvu na imara.

Muda: Miezi tano.

Mahali: Kituo Kikubwa cha Mafundisho cha Mashahidi wa Yehova, Patterson, New York.

Masomo ya Gileadi—Patterson, New York

Kujiandikisha: Ndugu na bibi zao, ndugu wasio na bibi na dada wasioolewa wanaotumikia katika utumishi fulani wa pekee wa wakati wote. Wamisionere ambao walikuwa hawajasoma masomo hayo, mapainia wa pekee, Wanabeteli, ao waangalizi wenye kusafiri na bibi zao wanaweza kualikwa na Halmashauri ya Tawi ili waende kusoma masomo hayo. Wale ambao wanaalikwa wanapaswa kujua kusema na kuandika Kiingereza.

Faida: Ndugu Lade na bibi yake Monique, ambao walitoka katika inchi ya Amerika na ambao wametumikia katika mugao wao kwa miaka mingi, wanasema hivi:

“Masomo ya Gileadi yalitutayarisha kuenda mahali popote duniani, sasa tuko tayari kutumika pamoja na ndugu zetu wapendwa.” (Ndugu Lade)

“Ninapata furaha kubwa wakati ninatumia mambo ambayo nimejifunza katika Neno la Mungu. Furaha hiyo inaonyesha kama Yehova anatupenda.” (Dada Monique)

MASOMO YA HUDUMA YA UFALME

Kusudi: Kuzoeza waangalizi wenye kusafiri, wazee, na watumishi wa huduma, ili waweze kusimamia na kuongoza mambo vizuri katika kutaniko. (Mdo. 20:28) Kwenye masomo hayo wanajifunza namna ya kushugulikia hali ambazo zinatokea sasa, tabia fulani, na mahitaji ya kutaniko. Masomo hayo yanafanywa kisha miaka fulani. Baraza Lenye Kuongoza ndilo linaamua kuhusu wakati.

Muda: Katika miaka ambayo imepita, muda wa masomo hayo umetofautiana.

Mahali: Kwa kawaida, kwenye Jumba la Ufalme la karibu ao kwenye Jumba la Mikusanyiko.

Kujiandikisha: Wazee na watumishi wa huduma wanajulishwa na mwangalizi wa muzunguko. Biro ya tawi inaalika pia waangalizi wenye kusafiri.

Faida: Ndugu Quinn anasema hivi: “Hata kama masomo hayo yanafundisha mambo mengi kwa muda mufupi, yanachochea wazee waendelee kuwa na furaha na waendelee kuwa wanaume wenye nguvu katika kazi ya Yehova. Wazee ambao wametumika kwa muda murefu na wapya, wote wanajifunza namna ya kuchunga kutaniko na kuwa na umoja “katika mawazo yaleyale.”

Ndugu Michael anasema hivi: “Mazoezi yaligusia mambo yote, ni kusema, yalituchochea tupendezwe zaidi na mambo ya kiroho, yalituonya kuhusu hatari mbalimbali na yakatutolea mashauri mazuri ambayo tunaweza kutumia ili kuchunga kutaniko.”

MASOMO YA WAANGALIZI WENYE KUSAFIRI NA BIBI ZAOi

Kusudi: Kusaidia waangalizi wa muzunguko waweze kutumikia vizuri zaidi makutaniko, wajikaze “kusema na kufundisha” kwa bidii, na pia waweze kuchunga vizuri kundi la Mungu.​—1 Tim. 5:17; 1 Pet. 5:2, 3.

Muda: Mwezi moja.

Mahali: Panachaguliwa na biro ya tawi.

Kujiandikisha: Biro ya tawi inawaalika waangalizi wenye kusafiri pamoja na bibi zao.

Faida: Ndugu Joel na bibi yake Connie ambao walialikwa kwenye darasa la 1 la masomo hayo katika mwaka wa 1999, walisema hivi: “Masomo hayo yalitusaidia tusamini sana namna Kristo anaongoza tengenezo na tuunge kabisa mukono uongozi wake. Pia tulijifunza kwamba ni jambo la lazima sana kuwatia ndugu moyo na kusaidia kila kutaniko liwe lenye umoja. Zaidi ya hayo, tulijifunza kwamba wakati mwangalizi mwenye kusafiri anatoa shauri ao anarekebisha jambo fulani, kusudi lake kubwa ni kusaidia ndugu waone kwamba Yehova anawapenda sana.

MASOMO YA NDUGU WA HALMASHAURI YA TAWI NA BIBI ZAO

Kusudi: Kusaidia ndugu wanaotumikia katika Halmashauri ya Tawi waweze kusimamia vizuri kazi ambayo inafanywa kwenye Beteli, waweze kuhangaikia kazi ambayo inafanywa katika makutaniko, na pia kuhangaikia waangalizi ambao wanatumikia katika maeneo mbalimbali.​—Lu. 12:48b.

Muda: Miezi mbili.

Mahali: Kituo Kikubwa cha Mafundisho cha Mashahidi wa Yehova, Patterson, New York.

Kujiandikisha: Halmashauri ya Utumishi ya Baraza Lenye Kuongoza inawaalika ndugu wa Halmashauri ya Tawi pamoja na bibi zao.

Faida: Ndugu Lowell na bibi yake Cara walikuwa kati ya wale ambao walialikwa kwenye darasa la 25. Na leo wanatumikia katika inchi ya Nijeria.

Ndugu Lowell anasema hivi: “Masomo hayo yalinikumbusha kwamba hata niwe na kazi nyingi sana ya kufanya, jambo la lazima zaidi ambalo ninapaswa kufanya ili nimufurahishe Yehova ni kuwa na hali nzuri ya kiroho.”

Cara anakumbuka somo ambalo alijifunza kwenye masomo hayo, anasema hivi: “Ikiwa siwezi kufasiria jambo fulani kwa urahisi, ninajifunza tena jambo hilo vizuri mbele ya kuwafundisha wengine.”

g Masomo haya hayajaanza kufanywa katika inchi zote.

h Masomo haya hayajaanza kufanywa katika inchi zote.

i Masomo haya hayajaanza kufanywa katika inchi zote.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine