Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 5 uku. 6
  • Kuko Malaika Wabaya?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuko Malaika Wabaya?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je, Roho Waovu Wako Kabisa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Kweli Juu ya Malaika
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Uasi Unatokea Mbinguni
    Roho za Wafu—Zinaweza Kukusaidia ao Kukutendea Mubaya? Zinakuwaka Kabisa?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 5 uku. 6
Malaika wabaya, ao mashetani

HABARI KUBWA | MALAIKA​—WAKO KABISA? SABABU GANI TUFIKIRIE JAMBO HILO?

Kuko Malaika Wabaya?

Ndiyo, kuko malaika wabaya. Walitoka wapi? Kumbuka kwamba Mungu aliumba malaika na uhuru wa kuchagua. Kisha tu kuumbwa kwa mwanaume na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Eva, kiumbe mumoja wa roho mwenye kuwa mukamilifu alitumia mubaya uhuru wake wa kuchagua na akaanzisha uasi katika dunia. Alifikia kuchochea Adamu na Eva wamuasi Mungu. (Mwanzo 3:1-7; Ufunuo 12:9) Biblia haionyeshe kama kiumbe huyo wa roho alikuwa na jina gani na kama alikuwa na cheo gani mbinguni mbele ya kuasi Mungu. Lakini kisha uasi wake, kwa kufaa Biblia inamuita Shetani, jina lenye kumaanisha “Mupinzani,” na Ibilisi, jina lenye kumaanisha “Musingiziaji.”​—Mathayo 4:8-11.

Jambo la huzuni ni kwamba uasi huo muovu haukuishia hapo. Katika siku za Noa, hesabu yenye haijulikane ya malaika ‘waliacha makao yao wenyewe’ katika familia ya mbinguni ya Mungu. Waliacha kusudi la kuumbwa kwao, wakakuja hapa duniani na kuvaa miili ya watu ili kufanya matendo mabaya sana.​—Yuda 6; Mwanzo 6:1-4; 1 Petro 3:19, 20.

Ni nini ilipata malaika hao wabaya? Wakati Mungu alileta garika katika dunia yote ili kuondoa ubaya, malaika hao walivaa tena miili yao ya kiroho na kurudia mbinguni. Lakini, Mungu hakuruhusu malaika hao wabaya warudie kwenye “mahali pao pa kwanza.” Lakini, aliwafungia katika hali ya chini ya “giza zito [la kiroho]” yenye kuitwa Tartaro. (Yuda 6; 2 Petro 2:4) Mashetani hao wamejitia chini ya utawala wa Shetani Ibilisi, ‘mutawala wa roho waovu,’ mwenye ‘anajigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru.’​—Mathayo 12:24; 2 Wakorintho 11:14.

Biblia inafundisha kwamba Ufalme wa Kimesiya, ni kusema serikali ya mbinguni, uliwekwa katika mwaka wa 1914.a Kisha tukio hilo la maana, Shetani na mashetani wake walifukuzwa kutoka mbinguni na wakatupwa kwenye ujirani wa dunia. Kuenea sana kwa uovu na mwenendo mubaya sana katika dunia kunashuhudia uvutano wao muovu.​—Ufunuo 12:9-12.

Lakini, kuongezeka kwa mwenendo mubaya na jeuri yenye kuchukiza kunahakikisha kwamba mwisho wa utawala wao wenye kuogopesha unakaribia. Hivi karibuni, malaika hao waovu watatiwa katika hali ya kutotenda. Kisha Ufalme wa Mungu kutawala dunia paradiso kwa miaka 1000, malaika hao wabaya watakuwa na nafasi mufupi ya mwisho ili kujaribu wanadamu. Kisha, wataharibiwa milele.​—Mathayo 25:41; Ufunuo 20:1-3, 7-10.

a Ili kupata habari zaidi kuhusu Ufalme wa Mungu, ona sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kinapatikana pia kwenye www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine