Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 1 uku. 19
  • Ulijua?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ulijua?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Onyesha Roho ya Upainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • “Ningewezaje . . . nisipoongozwa na mtu?”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 1 uku. 19
Filipo anakaa pembeni ya mwanaume Mwetiopia na iko namufasiria Maandiko, wako mu gari yenye kukokotwa na farasi yenye kuwa na magurudumu ine na kuko mutu mwenye iko naitembeza.

Ulijua?

Towashi Mwetiopia alikuwa mu gari ya aina gani wakati Filipo alimukaribia?

MU LUGA ya kwanza-kwanza, neno yenye kutafsiriwa “gari” mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya inaweza kumaanisha aina mbalimbali za gari. (Mdo. 8:28, 29, 38) Lakini, inaonekana kama gari yenye Mwetiopia alikuwa ndani ilikuwa kubwa zaidi kuliko gari yenye ilitumiwa mu vita ao mu mashindano. Ona juu ya nini tunasema vile.

Ule Mwetiopia alikuwa ofisa mukubwa na alisafiri safari ya murefu. Alikuwa “mwanaume mwenye alikuwa na mamlaka chini ya Kandake, malkia wa Waetiopia, na mwenye alikuwa anasimamia hazina yote ya malkia.” (Mdo. 8:27) Etiopia ya zamani ilitia ndani Sudan ya leo na sehemu kubwa ya kusini ya Misri ya leo. Hata kama inawezekana ule mwanaume hakusafiri mu gari ileile wakati wote wa safari, alipaswa kuwa na mizigo kwa ajili ya ile safari ya murefu. Kati ya magari yenye ilitumiwa mu karne ya kwanza ili kusafirisha watu, kulikuwa magari yenye kukokotwa na farasi yenye ilikuwa inafunikwa juu, na ilikuwa na magurudumu ine. Kulingana na kitabu Acts—An Exegetical Commentary, “magari ya vile iliruhusu mutu abebe mizigo mingi zaidi, asafiri muzuri zaidi, na pengine angeweza kuenda safari ya murefu.”

Ule Mwetiopia alikuwa nasoma wakati Filipo alimukaribia. Habari yenye kuwa mu Matendo inasema hivi: “Filipo akakimbia pembeni-pembeni na akamusikia [ule towashi] iko anasoma kwa sauti kubwa nabii Isaya.” (Mdo. 8:30) Magari ya kusafirisha watu yenye kukokotwa na farasi, haikutengenezwa ili iende mbio. Ule mwendo wa polepole ulisaidia ule towashi aweze kusoma, lakini pia ulisaidia Filipo akimbie na akute ile gari.

Ule Mwetiopia ‘aliomba Filipo apande na akae pamoja naye.’ (Mdo. 8:31) Ingekuwa gari ya mashindano, mwenye kuitembeza angesimama. Lakini mu gari ya kusafirisha watu, mulikuwa fasi kwenye towashi na Filipo wangeikala.

Kulingana na habari yenye kuongozwa na roho ya Mungu yenye kuwa mu Matendo sura ya 8 na ushuhuda mbalimbali wa kihistoria, hivi karibuni vichapo vyetu vimeonyesha towashi Mwetiopia iko mu gari yenye kukokotwa na farasi, yenye kuwa kubwa zaidi kuliko gari ya vita ao ya mashindano.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine