Kwa kiongozi juu ya Gitithi.+ Ya Asafu.
81 Mpigieni Mungu, nguvu zetu, vigelegele vya shangwe;+
Mpigieni Mungu wa Yakobo kelele za ushindi.+
2 Anzisheni muziki+ na kuchukua tari,+
Kinubi chenye kupendeza pamoja na kinanda.+
3 Katika mwezi mpya, pigeni baragumu;+
Katika mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+
4 Kwa maana ni sharti kwa ajili ya Israeli,+
Uamuzi wa hukumu wa Mungu wa Yakobo.
5 Alimwamuru Yosefu liwe kikumbusho,+
Alipokuwa akipita juu ya nchi ya Misri.+
Lugha ambayo sikuijua, niliendelea kuisikia.+
6 “Nililigeuza bega lake liondoke kwenye mzigo;+
Mikono yake ikaondoka kwenye kikapu.+
7 Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+
Nikaanza kukujibu katika mahali palipofichika pa mngurumo.+
Nikakuchunguza kando ya maji ya Meriba.+ Sela.
8 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu,+
Ee Israeli, ikiwa utanisikiliza.+
9 Katikati yako hakutakuwa na mungu yeyote mgeni;+
Wala hutamwinamia mungu wa kigeni.+
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,+
Yule anayekutoa katika nchi ya Misri.+
Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;+
Na Israeli hakuonyesha utayari wowote kunielekea.+
12 Na kwa hiyo nikawaacha waende katika ukaidi wa moyo wao;+
Wakatembea katika mashauri yao wenyewe.+
13 Laiti watu wangu wangekuwa wakinisikiliza,+
Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+
14 Adui zao ningewatiisha kwa urahisi,+
Nami ningegeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+
15 Na wale wanaomchukia Yehova vikali, watakuja kwake wakitetemeka,+
Na wakati wao utakuwa mpaka wakati usio na kipimo.
16 Naye ataendelea kumlisha mafuta ya ngano,+
Na kutokana na mwamba nitakushibisha asali.”+