Hosea
3 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Nenda tena, mpende mwanamke anayependwa na rafiki+ yako na ambaye anafanya uzinzi, kama vile Yehova alivyowapenda wana wa Israeli+ ingawa wanageukia miungu mingine+ na kupenda keki za zabibu kavu.”+
2 Nami nikajinunulia huyo mwanamke kwa vipande kumi na tano vya fedha+ na kipimo kimoja cha homeri ya shayiri na nusu homeri ya shayiri. 3 Ndipo nikamwambia: “Utakaa ukiwa wangu muda wa siku nyingi.+ Usifanye uasherati,+ nawe usiwe wa mwanamume mwingine;+ nami pia nitakuwa vivyo hivyo kwako.”
4 Hiyo ni kwa sababu wana wa Israeli watakaa muda wa siku nyingi bila mfalme+ wala mkuu wala dhabihu+ wala nguzo wala efodi+ wala terafimu.+ 5 Baadaye wana wa Israeli watarudi na hakika watamtafuta Yehova Mungu wao,+ na Daudi mfalme wao;+ nao watakuja kwa Yehova+ na kwa wema wake wakitetemeka katika siku za mwisho.+