Hosea
4 Sikieni neno la Yehova, enyi wana wa Israeli, kwa maana Yehova ana kesi na wakaaji wa nchi,+ kwa maana hakuna kweli+ wala fadhili zenye upendo wala kumjua Mungu katika nchi.+ 2 Kuna mambo ambayo yameenea, kutangaza laana+ na kuzoea kufanya udanganyifu+ na uuaji+ na wizi+ na uzinzi,+ na vitendo vya kumwaga damu vimegusana na vitendo vingine vya kumwaga damu.+ 3 Ndiyo sababu nchi itaomboleza+ na kila mkaaji ndani yake atadhoofika pamoja na mnyama wa mwituni na kiumbe kinachoruka cha mbinguni, na hata samaki wa baharini watakusanywa katika kifo.+
4 “Hata hivyo, mtu yeyote asishindane,+ wala mtu yeyote asikaripie, kwa maana watu wako ni kama wale wanaoshindana na kuhani.+ 5 Nawe hakika utajikwaa wakati wa mchana,+ na hata nabii atajikwaa pamoja nawe, kama wakati wa usiku.+ Nami nitamnyamazisha mama yako.+ 6 Hakika watu wangu watanyamazishwa, kwa sababu hakuna ujuzi.+ Kwa kuwa wewe mwenyewe umeukataa ujuzi,+ mimi pia nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu;+ na kwa sababu unaendelea kuisahau sheria ya Mungu wako,+ hata mimi nitawasahau wana wako.+ 7 Kulingana na wingi wao, ndivyo wamenitendea dhambi.+ Wamebadili utukufu wangu kuwa aibu tupu.+ 8 Wanazidi kula dhambi ya watu wangu, nao huendelea kuinua nafsi zao kwenye kosa lao.+
9 “Na itakuwa kwa watu kama vile itakavyokuwa kwa kuhani;+ nami hakika nitawatoza hesabu kwa sababu ya njia zao;+ nami nitarudisha matendo yao juu yao.+ 10 Nao watakula, lakini hawatashiba.+ Watawatendea wanawake kama makahaba; lakini hawataongezeka,+ kwa sababu wameacha kumjali Yehova.+ 11 Uasherati na divai na divai tamu ndivyo vinavyoondoa kusudi jema.+ 12 Watu wangu mwenyewe wanaendelea kuuliza habari+ kutoka kwa sanamu yao ya mti,+ na fimbo yao ya mkononi huwaambia; kwa maana roho ya uasherati imewafanya watange-tange,+ nao kwa uasherati hutoka chini ya Mungu wao.+ 13 Wao hutoa dhabihu juu ya vilele vya milima,+ nao hufukiza moshi wa dhabihu juu ya vilima,+ chini ya mti mnene na mlubna na mti mkubwa, kwa sababu kivuli chake ni kizuri.+ Ndiyo sababu binti zenu hufanya uasherati na binti-wakwe zenu hufanya uzinzi.
14 “Sitatoza hesabu juu ya binti zenu kwa sababu wanafanya uasherati, wala juu ya binti-wakwe zenu kwa sababu wanafanya uzinzi. Kwa maana, kwa habari ya wanaume, hujiendea zao wenyewe pamoja na makahaba,+ nao hutoa dhabihu pamoja na wanawake makahaba wa hekaluni;+ na watu ambao hawaelewi+ watakanyagiwa chini. 15 Ijapokuwa unafanya uasherati, Ee Israeli,+ Yuda asiwe na hatia,+ nanyi msije Gilgali,+ wala msiende Beth-aveni+ wala kuapa ‘Kama anavyoishi Yehova!’+ 16 Kwa maana, kama vile ng’ombe mkaidi, ndivyo Israeli amekuwa mkaidi.+ Je, ni wakati huu kwamba Yehova atawachunga kama vile mwana-kondoo dume katika mahali penye nafasi pana? 17 Efraimu ameshikamana na sanamu.+ Mwache!+ 18 Pombe yao ya ngano ikishamalizika,+ hakika wamemtendea mwanamke kama kahaba.+ Hakika wanaomkinga+ wamependa aibu.+ 19 Upepo umemfunika mabawa yake.+ Nao watapatwa na aibu kutokana na dhabihu zao.”+