Hosea
5 “Sikieni hili, enyi makuhani,+ na mkaze uangalifu, enyi nyumba ya Israeli, na ninyi, enyi nyumba ya mfalme,+ tegeni sikio, kwa maana hukumu hii inawahusu ninyi; kwa maana mmekuwa mtego+ katika Mispa na kama wavu uliotandazwa juu ya Tabori.+ 2 Na wale wanaoasi wamehusika sana+ katika kazi ya kuua, nami nilikuwa himizo kwao wote.+ 3 Mimi binafsi nimejua Efraimu,+ Israeli nayo haikufichwa kutoka kwangu.+ Kwa sasa, Ee Efraimu, umewatendea wanawake kama makahaba;+ Israeli imejitia unajisi.+ 4 Matendo yao hayawaruhusu kurudi kwa Mungu wao,+ kwa sababu kuna roho ya uasherati+ katikati yao; nao hawakumtambua Yehova.+ 5 Na kiburi cha Israeli kimeshuhudia mbele ya uso wake;+ na Israeli na Efraimu wamekwazwa katika kosa lao.+ Yuda pia amejikwaa pamoja nao.+ 6 Walienda kumtafuta Yehova wakiwa na makundi yao na mifugo yao, lakini hawakuweza kumpata.+ Alikuwa amejiondoa kwao. 7 Wamemtendea hila+ Yehova mwenyewe, kwa maana wamezaa wana wa kigeni.+ Sasa, mwezi mmoja utawameza pamoja na mafungu yao ya mashamba.+
8 “Pigeni baragumu+ katika Gibea,+ tarumbeta katika Rama! Pigeni kelele za vita katika Beth-aveni+—nyuma yako, Ee Benyamini!+ 9 Ee Efraimu, utakuwa kitu cha kushangaza katika siku ya kukemewa.+ Nimejulisha maneno yenye kutegemeka+ kati ya makabila ya Israeli. 10 Wakuu wa Yuda wamekuwa kama watu wanaosogeza nyuma mpaka.+ Nitamwaga ghadhabu yangu kama maji juu yao. 11 Efraimu ameonewa, amepondwa kwa haki,+ kwa maana alikuwa amejiamulia mwenyewe kumfuata adui yake.+ 12 Nami nilikuwa kama nondo+ kwa Efraimu na kama kuoza kwa nyumba ya Yuda.
13 “Na Efraimu akaona ugonjwa wake, na Yuda kidonda chake.+ Ndipo Efraimu akaenda Ashuru+ na kupeleka ujumbe kwa mfalme mkuu.+ Lakini huyo hakuweza kuwaponya ninyi,+ wala kuwaondolea kidonda kwa dawa yoyote.+ 14 Kwa maana mimi nitakuwa kama mwana-simba kwa Efraimu+ na kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni kwa nyumba ya Yuda. Mimi, mimi mwenyewe nitararua vipande-vipande nami nitaenda na kuchukulia mbali, na hapatakuwa na mkombozi.+ 15 Nitaenda, nitarudi mahali pangu mpaka watakapoibeba hatia yao;+ nao hakika watautafuta uso wangu.+ Watanitafuta,+ wanapokuwa katika dhiki kali.”+