Tito
2 Hata hivyo, wewe fuliza kusema mambo yote yale yafaayo kwa fundisho lenye afya. 2 Acha wanaume wenye umri mkubwa wawe wenye kiasi katika mazoea, wachukua-mambo kwa uzito, timamu katika akili, wenye afya katika imani, katika upendo, katika uvumilivu. 3 Hivyohivyo acha wanawake wenye umri mkubwa wawe wenye kuhofu Mungu katika tabia, si wachongezi, wala waliofanywa watumwa wa divai nyingi sana, walimu wa lililo jema; 4 ili wapate kuwatia akili wanawake vijana kuwapenda waume zao, kuwapenda watoto wao, 5 kuwa timamu katika akili, safi kiadili, wafanyakazi nyumbani, wema, wakijitiisha wenyewe kwa waume zao wenyewe, ili neno la Mungu lisipate kusemewa kwa maneno yenye kuudhi.
6 Hivyohivyo fuliza kuwahimiza kwa bidii wanaume vijana zaidi wawe timamu katika akili, 7 katika mambo yote ukijionyesha mwenyewe kuwa kielelezo cha kazi zilizo bora; ukionyesha kutofisidika katika fundisho lako, uchukuaji wa mambo kwa uzito, 8 usemi wenye afya usioweza kulaumiwa; ili mtu aliye upande wenye kupinga apate kuaibika, akiwa hana jambo lolote ovu la kusema juu yetu. 9 Acha watumwa wawe katika ujitiisho kwa wamiliki wao wenyewe katika mambo yote, na kuwapendeza vema, si kujibu kwa ujeuri, 10 si kufanya wizi, bali kuonyesha wazi uaminifu mwema kwa ukamili, ili wapate kuremba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote.
11 Kwa maana fadhili isiyostahiliwa ya Mungu iletayo wokovu kwa watu wa namna zote imedhihirishwa, 12 ikituagiza tukatae katakata kukosa kumwogopa Mungu na tamaa za kilimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji-kimungu katikati ya mfumo uliopo wa mambo, 13 huku tukingoja tumaini lenye furaha na udhihirisho wenye utukufu wa Mungu mkuu na wa Mwokozi wetu, Kristo Yesu, 14 aliyejitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili apate kutukomboa sisi kutoka kwenye kila namna ya uasi-sheria na kujisafishia mwenyewe watu walio wake mwenyewe pekee, wenye bidii kwa kazi zilizo bora.
15 Fuliza kusema mambo haya na kuhimiza kwa bidii na kukaripia kwa mamlaka kamili ya kuamuru. Usiache kamwe mtu yeyote akudharau.