Tito
Kwa Tito
1 Paulo, mtumwa wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kulingana na imani ya wachaguliwa wa Mungu na ujuzi sahihi wa kweli ambayo yapatana na ujitoaji-kimungu 2 juu ya msingi wa tumaini la uhai udumuo milele ambao Mungu, asiyeweza kusema uwongo, aliahidi kabla ya nyakati zinazodumu muda mrefu, 3 lakini katika nyakati zake mwenyewe zipasazo alifanya neno lake liwe dhahiri katika kuhubiri ambako mimi nilikabidhiwa, chini ya amri ya Mwokozi wetu, Mungu; 4 kwa Tito, mtoto halisi kulingana na imani ambayo yashirikiwa:
Na kuwe fadhili isiyostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Mwokozi wetu.
5 Kwa sababu hii nilikuacha wewe Krete, ili upate kusahihisha mambo yaliyokuwa yenye kasoro na upate kuweka rasmi wanaume wazee katika jiji baada ya jiji, kama nilivyokupa wewe maagizo; 6 ikiwa kuna mtu yeyote asiye na shtaka, mume wa mke mmoja, mwenye watoto wanaoamini ambao hawakuwa chini ya shtaka la ufasiki wala la kuwa wasiotawalika. 7 Kwa maana mwangalizi lazima awe bila shtaka kama msimamizi-nyumba wa Mungu, si mwenye kufuata nia yake mwenyewe, si mwenye elekeo la kuwa na hasira ya kisasi, si mwenye fujo ya ulevi, si mpiga-watu, si mwenye pupa ya pato lisilo la haki, 8 bali mkaribishaji-wageni, mpenda-wema, timamu katika akili, mwadilifu, mwaminifu-mshikamanifu, mwenye kujidhibiti, 9 mwenye kushika kwa imara lile neno la uaminifu kwa habari ya usanifu wa kufundisha kwake, ili apate kuwa aweza kuhimiza kwa bidii kwa fundisho lililo lenye afya na pia kukaripia wale ambao hupinganisha.
10 Kwa maana kuna watu wengi wasiotawalika, waongeaji wa yasiyokuwa na faida, na wadanganyi wa akili, hasa watu wale ambao hushikamana sana na tohara. 11 Ni lazima kufunga vinywa vya hao, kwa kuwa watu haohao hufuliza kupindua watu wa nyumba nzima-nzima kwa kufundisha mambo wasiyopaswa kwa ajili ya pato lisilo la haki. 12 Mtu fulani kati yao, nabii wao wenyewe, alisema: “Wakrete ni waongo sikuzote, hayawani-mwitu wabaya, walafi wasioajiriwa kazi.”
13 Ushahidi huu ni kweli. Kwa sababu hiyohiyo fuliza kuwakaripia kwa ukali, ili wapate kuwa wenye afya katika imani, 14 bila kukazia uangalifu hekaya za Kiyahudi na amri za watu ambao hujigeuza mbali wenyewe kutoka kwenye kweli. 15 Vitu vyote ni safi kwa watu safi. Lakini kwa watu waliotiwa unajisi na wasio na imani hakuna kitu chochote kilicho safi, bali akili zao na pia dhamiri zao zimetiwa unajisi. 16 Wao hutangaza hadharani wamjua Mungu, lakini wao humkana yeye kwa kazi zao, kwa sababu ni wa kuchukiza na wasiotii na waliokataliwa kwa ajili ya kazi njema ya namna yoyote.