Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Wa Daudi.
61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba msaada.
Sikiliza sala yangu.+
 2 Nitakulilia kwa sauti kutoka katika miisho ya dunia
Ninapovunjika moyo.+
Niongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi.+
 3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,
Mnara ulio imara unaonilinda dhidi ya adui.+
 4 Nitakuwa mgeni katika hema lako milele;+
Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)
 5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia nadhiri zangu.
Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+
 6 Utamwongezea mfalme siku za maisha yake,+
Na miaka yake itatoka kizazi hadi kizazi.
 7 Ataketi kwenye kiti cha ufalme milele mbele za Mungu;+
Mpe upendo wako mshikamanifu na uaminifu, ili vimlinde.+
 8 Kisha nitaliimbia sifa jina lako milele+
Ninapotimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+