14 “Mwishowe utakapoingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, nawe uwe umeimiliki na kukaa ndani yake,+ nawe uwe umesema, ‘Acha niweke mfalme juu yangu kama mataifa yote yanayonizunguka’;+
15 utaweka juu yako mfalme ambaye Yehova Mungu wako atachagua.+ Kutoka katikati ya ndugu zako utaweka mfalme juu yako. Hutaruhusiwa kuweka juu yako mgeni ambaye si ndugu yako.
19 Lakini ninyi—leo mmemkataa Mungu+ wenu ambaye alikuwa mwokozi wenu kutoka katika maovu yenu yote na taabu zenu, nanyi mkasema: “Hapana, bali uweke mfalme juu yetu.” Basi sasa simameni mbele za Yehova kulingana na makabila+ yenu na kulingana na maelfu yenu.’”