3Naye Musa akawa mchungaji wa kundi la Yethro,+ kuhani wa Midiani, aliyekuwa mwana-mkwe wake.+ Alipokuwa akiliongoza kundi kuelekea upande wa magharibi wa nyika, mwishowe akafika kwenye mlima wa Mungu wa kweli,+ Horebu.+
18 Sasa watu wote walikuwa wakiona ile mingurumo na miwako ya umeme na sauti ya baragumu na mlima ukitoa moshi. Watu walipoona hilo, ndipo wakatetemeka na kusimama mbali.+
16 Na utukufu+ wa Yehova ukaendelea kukaa juu ya Mlima Sinai,+ nalo wingu likaendelea kuufunika kwa siku sita. Mwishowe katika siku ya saba akamwita Musa kutoka katikati ya lile wingu.+
8 Basi akaamka, akala na kunywa, naye akazidi kwenda katika nguvu za chakula kile kwa siku 40,+ mchana na usiku, mpaka Horebu, mlima wa Mungu wa kweli.+