8 Mwishowe Farao akawaita Musa na Haruni na kusema: “Msihi Yehova+ ili awaondoe vyura hawa kutoka kwangu na kwa watu wangu, kwa maana nataka kuwaruhusu watu waende zao, wakamtolee Yehova dhabihu.”+
28 Msihi Yehova ili mingurumo hii ya Mungu na mvua yake ya mawe+ ziishie hapo. Ndipo nitakuwa tayari kuwaruhusu mwende zenu, nanyi hamtaendelea kukaa zaidi.”
19 Na watu wote wakaanza kumwambia Samweli: “Sali+ kwa Yehova Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, kwa maana hatutaki kufa; kwa sababu tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu zote kwa kujiombea mfalme.”