4 Na Farao hatawasikiliza ninyi;+ nami nitalazimika kuuweka mkono wangu juu ya Misri na kuleta majeshi yangu,+ watu wangu,+ wana wa Israeli,+ kutoka katika nchi ya Misri kwa hukumu kubwa.+
19 Basi makuhani wenye kufanya uchawi wakamwambia Farao: “Ni kidole+ cha Mungu!”+ Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mkaidi,+ naye hakuwasikiliza, kama vile Yehova alivyokuwa amesema.
7 Na watu wa Ashdodi wakaona kwamba iko hivyo, ndipo wakasema: “Msiache sanduku la Mungu wa Israeli likae pamoja nasi, kwa sababu mkono wake umekuwa mzito juu yetu na juu ya Dagoni mungu wetu.”+
11 Hivyo, basi, tazama! mkono wa Yehova uko juu yako wewe, nawe utakuwa kipofu, usiweze kuiona nuru ya jua kwa kipindi fulani.” Mara moja ukungu mzito na giza vikamwangukia, naye akazunguka akitafuta watu wa kumwongoza wakiwa wamemshika mkono.+