8 Basi Yehova akauacha moyo wa Farao mfalme wa Misri uwe mkaidi,+ naye akawafuatilia wana wa Israeli, huku wana wa Israeli wakienda kwa mkono ulioinuliwa.+
30 Naye Sihoni mfalme wa Heshboni hakuturuhusu tupite katikati yake, kwa sababu Yehova Mungu wako alikuwa ameiacha roho yake iwe kaidi+ na moyo wake uwe mgumu, ili amtie mkononi mwako kama ilivyo leo hii.+
20 Kwa kuwa hiyo ndiyo iliyokuwa njia ya Yehova ya kutenda, kuacha mioyo yao iwe migumu+ ili watangaze vita juu ya Israeli, kusudi awaangamize, ili wasipate kibali,+ bali ili yeye apate kuwaangamiza, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.+
6 Pia, kwa nini mfanye mioyo yenu kuwa migumu kama vile Misri na Farao walivyofanya mioyo yao kuwa migumu?+ Je, haikuwa ni mara tu Yeye alipowatendea vikali+ ndipo walipowaachilia waende zao, nao wakaenda zao?+