Zaburi
Kwa kiongozi wa Yeduthuni.+ Muziki wa Daudi.
39 Nilisema: “Nitalinda njia zangu+
Ili nisiendelee kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+
Nitaweka lijamu kama mlinzi wa kinywa changu mwenyewe,+
Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”+
2 Nikawa asiyeweza kusema kwa kukaa kimya;+
Nikaendelea kulinyamazia lililo jema,+
Na kuumia kwangu kukatengwa.
3 Moyo wangu ukawa na moto ndani yangu;+
Wakati wa kuugua kwangu moto ukaendelea kuwaka.
Nilisema kwa ulimi wangu:
4 “Ee Yehova, nijulishe mwisho wangu,+
Na kipimo cha siku zangu—ni kipimo gani,+
Ili nipate kujua kadiri nilivyo wa muda mfupi.+
5 Tazama! Umezifanya siku zangu kuwa chache tu;+
Na urefu wa maisha yangu si kitu mbele zako.+
Kwa kweli kila mtu wa udongo, ingawa anasimama imara, si kitu ila pumzi tu.+ Sela.
6 Kwa kweli mtu hutembea huku na huku kama kivuli tu.+
Kwa kweli wana msukosuko ambao ni ubatili.+
Mmoja anarundika vitu wala hajui ni nani atakayevikusanya.+
7 Na sasa, nimetumainia nini, Ee Yehova?
Matarajio yangu yanakuelekea wewe.+
9 Niliendelea kuwa asiyeweza kusema;+ sikuweza kufungua kinywa changu,+
Kwa maana wewe mwenyewe ulichukua hatua.+
11 Umemrekebisha mtu kwa makaripio dhidi ya kosa,+
Nawe unakula vitu vyake vyenye kutamanika kama nondo.+
Kwa kweli kila mtu wa udongo ni pumzi tu.+ Sela.