Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi, muziki.
40 Nilimtumainia Yehova kwa bidii,+
Kwa hiyo akanitegea sikio lake na kusikia kilio changu cha kuomba msaada.+
2 Yeye pia akaniinua kutoka katika shimo lenye kunguruma,+
Kutoka katika matope ya nchi.+
Kisha yeye akainua miguu yangu juu ya mwamba;+
Akazifanya imara hatua zangu.+
3 Tena, akatia wimbo mpya katika kinywa changu,
Sifa kwa Mungu wetu.+
Wengi wataona hilo na kuogopa,+
Nao watamtegemea Yehova.+
4 Mwenye furaha ni mwanamume ambaye amemfanya Yehova kuwa tegemeo lake+
Na ambaye hakuelekeza uso wake kwa watu wakaidi,
Wala kwa wale wanaogeukia uwongo.+
5 Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi,+
Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea;+
Hakuna wa kulinganishwa nawe.+
Ikiwa ningetaka kueleza na kusema juu yake,
Zimekuwa nyingi sana kuliko vile ninavyoweza kusimulia.+
6 Hukupendezwa na dhabihu na toleo;+
Haya masikio yangu uliyafungua.+
Hukutaka toleo la kuteketezwa na toleo la dhambi.+
9 Nimetangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+
Tazama! Siizuii midomo yangu.+
Ee Yehova, wewe mwenyewe unajua hivyo vema.+
10 Uadilifu wako sikuufunika moyoni mwangu.+
Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.+
Sikuficha fadhili zako zenye upendo na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+
11 Wewe mwenyewe, Ee Yehova, usinizuilie huruma zako.+
Fadhili zako zenye upendo na ukweli wako zinilinde daima.+
12 Kwa maana misiba ilinizunguka mpaka ikawa haihesabiki.+
Makosa yangu mengi zaidi yalinifikia kuliko vile nilivyoweza kuona;+
Yakawa mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,+
Nao moyo wangu mwenyewe uliniacha.+
14 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+
Wale wanaoitafuta nafsi yangu wapate kuifagilia mbali.+
Wale wanaopendezwa na msiba wangu na wageuke na kufedheheshwa.+