Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 14:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nao wakamwambia Musa: “Je, ni kwa sababu hakuna makaburi yoyote huko Misri ndiyo sababu umetuleta hapa ili tufie nyikani?+ Ni nini hiki ambacho umetutendea kwa kutuongoza kutoka Misri?

  • Kutoka 16:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Na wana wa Israeli wakawa wakiwaambia: “Laiti tungekufa+ kwa mkono wa Yehova katika nchi ya Misri tulipokuwa tukiketi kando ya vyungu vya nyama,+ tulipokuwa tukila mkate na kushiba, kwa sababu ninyi mmetutoa na kutuleta nyikani ili kuliua kutaniko lote kwa njaa.”+

  • Hesabu 14:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Na kwa nini Yehova anatuleta kwenye nchi hii ili tuanguke kwa upanga?+ Wake zetu na watoto wetu wadogo watakuwa nyara.+ Je, si afadhali kwetu turudi Misri?”+

  • Nehemia 9:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo wakakataa kusikiliza,+ wala hawakuyakumbuka+ matendo yako ya ajabu ambayo ulikuwa umewafanyia, bali wakafanya shingo zao kuwa ngumu+ na kujichagulia mkuu+ ili kurudi kwenye hali yao ya utumwa katika Misri. Lakini wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe,+ mwenye neema+ na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi+ wa fadhili zenye upendo, nawe hukuwaacha.+

  • Matendo 7:39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 39 Mababu zetu walikataa kumtii, bali wakamsukuma kando+ na katika mioyo yao wakageuka kurudi Misri,+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki