13 “Wewe nawe, nena na wana wa Israeli, na kusema, ‘Hasa sabato zangu, mtazishika,+ kwa maana ni ishara kati yangu na ninyi katika vizazi vyenu ili mpate kujua kwamba mimi Yehova ninawatakasa ninyi.+
15 Nawe ukumbuke kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri+ na Yehova Mungu wako akakutoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa.+ Ndiyo sababu Yehova Mungu wako alikuamuru uendelee kuishika siku ya sabato.+
22 Nanyi msitoe mzigo wowote katika nyumba zenu siku ya sabato; wala msifanye kazi yoyote.+ Nanyi mwitakase siku ya sabato, kama nilivyowaamuru mababu zenu;+
15 Hata hivyo, Bwana akamjibu na kusema: “Wanafiki,+ je, kila mmoja wenu siku ya sabato hafungui ng’ombe wake au punda wake kutoka kwenye kibanda na kumpeleka akamnyweshe?+