12 Na wana wa Israeli hawataweza kusimama juu ya adui zao.+ Watawageuzia mgongo adui zao, kwa sababu wamekuwa kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuharibiwa. Sitakuwa pamoja nanyi tena isipokuwa mharibu kutoka katikati yenu kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuharibiwa.+
14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakaanza kuwapora;+ naye akawauza mkononi mwa adui zao waliowazunguka pande zote,+ wala hawakuweza tena kusimama mbele ya adui zao.+
4 isipokuwa iwe kwamba mtu atainama chini ya wafungwa na kwamba watu wataendelea kuanguka chini ya wale ambao wameuawa?+ Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa.+
10 Kwa maana ikiwa mngelipiga na kuliua jeshi lote la Wakaldayo wanaopigana nanyi+ na kati yao wabaki watu waliochomwa,+ kila mmoja wao angesimama katika hema lake na kuliteketeza jiji hili kwa moto.”’”