3 Kaa ukiwa mgeni katika nchi hii,+ nami nitaendelea kuwa pamoja nawe na kukubariki, kwa sababu nitakupa wewe na uzao wako nchi zote hizi,+ nami nitaitimiza ahadi yenye kiapo ambayo nilimwapia Abrahamu baba yako,+
24 Mwishowe Yosefu akawaambia ndugu zake: “Ninakufa; lakini Mungu hatakosa kuwaelekezea fikira zake,+ naye kwa hakika atawatoa katika nchi hii na kuwapeleka mpaka nchi ambayo aliwaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”+
5 Na itakuwa kwamba Yehova atakapokuwa amekuingiza katika nchi ya Wakanaani na Wahiti na Waamori na Wahivi na Wayebusi,+ ambayo aliwaapia mababu zako kuwa atakupa,+ nchi inayotiririka maziwa na asali,+ ndipo utatoa utumishi huu katika mwezi huu.