22 Nami nitakutokea hapo na kusema nawe toka juu ya kifuniko+ hicho, toka katikati ya wale makerubi wawili walio juu ya sanduku la ushuhuda, naam, yote nitakayokuamuru wewe kwa ajili ya wana wa Israeli.+
42 Ni toleo la daima+ la kuteketezwa katika vizazi vyenu vyote kwenye mwingilio wa hema la mkutano mbele za Yehova, ambapo nitajitokeza kwenu ili kusema nanyi hapo.+
36 Nawe utaponda sehemu yake iwe unga laini na kutia kiasi chake fulani mbele ya ule Ushuhuda katika hema la mkutano,+ nitakapojitokeza kwako.+ Yatakuwa matakatifu zaidi kwenu.
2 Na Yehova akamwambia Musa: “Sema na Haruni ndugu yako, asiwe akija nyakati zote katika mahali patakatifu+ ndani ya pazia,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya Sanduku, asije akafa;+ kwa sababu nitaonekana katika wingu+ juu ya kifuniko+ hicho.