Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 30:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nawe utaiweka mbele ya pazia lililo karibu na sanduku la ushuhuda,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya ule Ushuhuda, mahali ambapo nitajitokeza kwako.+

  • Mambo ya Walawi 16:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Na Yehova akamwambia Musa: “Sema na Haruni ndugu yako, asiwe akija nyakati zote katika mahali patakatifu+ ndani ya pazia,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya Sanduku, asije akafa;+ kwa sababu nitaonekana katika wingu+ juu ya kifuniko+ hicho.

  • Hesabu 7:89
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 89 Sasa wakati wowote ambapo Musa aliingia ndani ya hema la mkutano ili kusema naye,+ ndipo aliposikia sauti ikizungumza naye toka juu ya kifuniko+ kilichokuwa juu ya sanduku la ushuhuda, kutoka katikati ya wale makerubi+ wawili; naye akasema naye.

  • Waamuzi 20:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kisha wana wa Israeli wakauliza kutoka kwa Yehova,+ kwa kuwa hapo ndipo lilipokuwa lile sanduku la agano+ la Mungu wa kweli siku hizo.

  • Zaburi 80:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 80 Ee Mchungaji wa Israeli, tega sikio,+

      Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi.+

      Wewe unayeketi juu ya makerubi,+ uangaze.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki