47 nao warudiwe na fahamu zao katika nchi ile ambayo wamechukuliwa mateka,+ nao hakika warudi+ na kutoa kwako ombi+ la kutaka kibali katika nchi ya watekaji wao,+ wakisema, ‘Tumetenda dhambi+ na kukosea,+ tumetenda uovu’;+
9 Mtakaporudi kwangu+ na kuzishika amri zangu+ na kuzifanya,+ hata watu wenu waliotawanywa wawe katika mwisho wa mbingu, kutoka huko nitawakusanya+ na kuwaleta+ mahali ambapo nimepachagua ili jina langu likae hapo.’+
13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu;+ rudini kwa Yehova Mungu wenu, kwa maana yeye ana neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ naye hakika atajuta kwa sababu ya msiba huo.+