Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 13:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Nitakasie kila mzaliwa wa kwanza wa kiume anayefungua kila tumbo la uzazi kati ya wana wa Israeli, kati ya wanadamu na wanyama. Ni wangu.”+

  • Kutoka 34:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Kila kitu ambacho kinafungua kwanza tumbo la uzazi ni changu,+ nayo mifugo yako yote, mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe-dume na wa kondoo.+

  • Mambo ya Walawi 27:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “‘Ila mzaliwa wa kwanza kati ya wanyama, anayezaliwa akiwa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya Yehova,+ mtu yeyote asimtakase. Awe ni ng’ombe au kondoo, ni wa Yehova.+

  • Hesabu 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Katika siku niliyompiga na kumuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ nilijitakasia kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia mwanadamu mpaka mnyama.+ Wanapaswa kuwa wangu. Mimi ni Yehova.”

  • Hesabu 18:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “Kila kitu kinachofungua tumbo la uzazi,+ cha kila namna yenye mwili, ambacho watamtolea Yehova, kati ya wanadamu na kati ya wanyama, kinapaswa kuwa chako. Hata hivyo, unapaswa kumkomboa mzaliwa wa kwanza wa wanadamu;+ na mzaliwa wa kwanza wa mnyama ambaye si safi unapaswa kumkomboa.+

  • Hesabu 18:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Ila tu ng’ombe-dume aliye mzaliwa wa kwanza au mwana-kondoo dume aliye mzaliwa wa kwanza au mbuzi aliye mzaliwa wa kwanza hutawakomboa.+ Hao ni kitu kitakatifu. Damu+ yao unapaswa kuinyunyiza juu ya madhabahu, na mafuta yao utayafukiza kama toleo linalotolewa kwa njia ya moto ili kuwa harufu ya kumtuliza Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki