31 “Nami nitauweka mpaka wako kutoka Bahari Nyekundu hadi bahari ya Wafilisti na kutoka nyikani hadi kwenye Mto;+ kwa sababu nitawaweka wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, na hakika wewe utawafukuzia mbali kutoka mbele yako.+
44 Tena Yehova akawapa pumziko+ kuwazunguka pande zote, kulingana na kila kitu ambacho alikuwa amewaapia+ mababu zao, wala hakuna mmoja kati ya adui zao wote aliyesimama mbele yao.+ Yehova aliwatia adui zao wote mkononi mwao.+
24 Basi wana wao+ wakaingia, wakaichukua nchi hiyo na kuimiliki,+ nawe ukatiisha+ mbele yao wakaaji wa nchi hiyo, Wakanaani,+ na kuwatia mikononi mwao, pamoja na wafalme+ wao na vikundi vya watu wa nchi,+ ili wawatendee kulingana na mapenzi yao.+