Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Sitawafukuza kutoka mbele yako kwa mwaka mmoja, ili nchi isiwe mahame yenye ukiwa nao wanyama wa mwituni waongezeke kwelikweli juu yako.+

  • Hesabu 33:55
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 55 “‘Hata hivyo, ikiwa hamtawafukuzia mbali wakaaji wa nchi hiyo kutoka mbele yenu,+ basi wale mtakaoacha watakuwa kama michomo katika macho yenu na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika nchi ambamo mtakuwa mkikaa.+

  • Kumbukumbu la Torati 7:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Na Yehova Mungu wako atayasukumia mbali mataifa haya toka mbele yako kidogo kidogo.+ Hutaruhusiwa kuwamaliza kabisa upesi, wanyama wa mwituni wasije wakaongezeka dhidi yako.

  • Yoshua 23:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 mnapaswa kujua hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyanyang’anya mataifa haya miliki yao kwa ajili yenu;+ nayo yatakuwa kwenu kama mtego na mnaso na kama kiboko mbavuni mwenu+ na kama miiba machoni penu mpaka mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa ninyi.+

  • Waamuzi 1:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Wala Efraimu hakuwafukuza Wakanaani waliokuwa wakikaa Gezeri, lakini Wakanaani waliendelea kukaa kati yao katika Gezeri.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki