15 Na ikawa kwamba, katika siku ya nne wakaanza kumwambia mke wa Samsoni: “Mdanganye mume wako ili atutegulie kitendawili hicho.+ Kama sivyo tutakuteketeza kwa moto+ wewe na nyumba ya baba yako. Je, mlitualika hapa ili mchukue mali zetu?”+
6 Na Wafilisti wakaanza kusema: “Ni nani aliyefanya jambo hili?” Ndipo wakasema: “Ni Samsoni mwana-mkwe wa yule Mtimna, kwa sababu alimchukua mke wake, akampa rafiki yake.”+ Kwa hiyo Wafilisti wakaenda na kumteketeza kwa moto mwanamke huyo na baba yake.+
10 Basi Amazia akawatenga, yaani, yale majeshi yaliyomjia kutoka Efraimu, ili waende kwao. Hata hivyo, hasira yao ikawaka sana juu ya Yuda, nao wakarudi kwao wakiwaka hasira.+