Zaburi 37:8 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 8 Acha hasira na uache ghadhabu;+Usijionyeshe umewaka hasira ili tu kufanya uovu.+ Methali 14:17 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 17 Yule anayekasirika upesi atatenda upumbavu,+ lakini mtu mwenye uwezo wa kufikiri huchukiwa.+ Methali 14:29 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 29 Yule ambaye si mwepesi wa hasira ana utambuzi mwingi,+ lakini anayekosa subira anainua upumbavu.+ Methali 27:4 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 4 Kuna ukatili wa ghadhabu, pia furiko la hasira,+ lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?+