27 Kwa hiyo Daudi akaondoka pamoja na watu wake, akapiga+ watu mia mbili kati ya Wafilisti, na Daudi akaleta magovi yao,+ akampa mfalme hesabu yake kamili, ili kufanya mapatano ya ndoa na mfalme. Naye Sauli akampa Mikali binti yake awe mke wake.+
11 Baadaye Sauli akatuma wajumbe+ kwa nyumba ya Daudi ili wailinde na kumuua asubuhi;+ lakini Mikali mke wake akamwambia Daudi, akisema: “Usipoiponya nafsi yako usiku wa leo, kesho utakuwa mtu aliyeuawa.”
29 Na ikawa kwamba wakati sanduku la agano+ la Yehova lilipokuja mpaka Jiji la Daudi, Mikali,+ binti ya Sauli, akaangalia chini kutoka dirishani, akamwona Mfalme Daudi akirukaruka na kusherehekea;+ naye akaanza kumdharau+ moyoni mwake.