1 Mambo ya Nyakati
15 Naye akaendelea kujijengea nyumba+ katika Jiji la Daudi; naye akatayarisha mahali+ kwa ajili ya sanduku la Mungu wa kweli na kulisimamishia hema. 2 Ndipo Daudi aliposema: “Mtu yeyote asilibebe sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua hao ili walibebe sanduku la Yehova+ na kumhudumia+ mpaka wakati usio na kipimo.” 3 Kisha Daudi akawakutanisha Israeli wote katika Yerusalemu+ ili kulipandisha sanduku+ la Yehova mpaka mahali pake ambapo alikuwa amelitayarishia.
4 Na Daudi akawakusanya wana wa Haruni+ na Walawi; 5 wa wana wa Kohathi, Urieli+ mkuu na ndugu zake, 120; 6 wa wana wa Merari,+ Asaya+ mkuu na ndugu zake, 220; 7 wa wana wa Gershomu,+ Yoeli+ mkuu na ndugu zake, 130; 8 wa wana wa Elisafani,+ Shemaya+ mkuu na ndugu zake, 200; 9 wa wana wa Hebroni, Elieli mkuu na ndugu zake, 80; 10 wa wana wa Uzieli,+ Aminadabu mkuu na ndugu zake, 112. 11 Tena, Daudi akawaita Sadoki+ na Abiathari+ makuhani, na Walawi Urieli,+ Asaya+ na Yoeli,+ Shemaya+ na Elieli+ na Aminadabu, 12 naye akawaambia: “Ninyi ndio vichwa+ vya upande wa baba vya Walawi. Jitakaseni,+ ninyi na ndugu zenu, nanyi mlipandishe sanduku la Yehova, Mungu wa Israeli mpaka mahali ambapo nimelitayarishia. 13 Kwa sababu mara ya kwanza hamkufanya hivyo,+ Yehova, Mungu wetu, alitulipukia,+ kwa kuwa hatukumtafuta kulingana na desturi.”+ 14 Basi makuhani na Walawi wakajitakasa+ ili walipandishe sanduku la Yehova, Mungu wa Israeli.
15 Ndipo wana wa Walawi wakaanza kulibeba+ sanduku la Mungu wa kweli, kama Musa alivyoamuru kwa amri ya Yehova, juu ya mabega yao na fimbo zikiwa juu yao.+ 16 Daudi akawaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji+ wakiwa na vyombo vya nyimbo,+ vinanda+ na vinubi+ na matoazi,+ wakipiga kwa sauti ili sauti ya kushangilia itokee.
17 Basi Walawi wakamweka Hemani+ mwana wa Yoeli na, kati ya ndugu zake, Asafu+ mwana wa Berekia; na, kati ya ndugu zao wana wa Merari, Ethani+ mwana wa Kushaya; 18 na pamoja nao ndugu zao wa mgawanyo wa pili,+ Zekaria,+ Beni na Yaazieli na Shemiramothi na Yehieli na Uni, Eliabu na Benaya na Maaseya na Matithia na Elifelehu na Mikneya, na Obed-edomu+ na Yeieli watunza-malango, 19 na waimbaji Hemani,+ Asafu+ na Ethani, wakiwa na matoazi ya shaba ili kuyapiga kwa sauti;+ 20 na Zekaria na Azieli+ na Shemiramothi na Yehieli na Uni na Eliabu na Maaseya na Benaya wakiwa na vinanda vilivyorekebishwa kupatana na sauti ya Alamothi,+ 21 na Matithia+ na Elifelehu na Mikneya na Obed-edomu na Yeieli na Azazia wakiwa na vinubi+ vilivyorekebishwa kupatana na Sheminithi,+ wawe viongozi; 22 na Kenania+ mkuu wa Walawi juu ya uchukuzi, yeye akitoa maagizo katika kuchukua, kwa maana alikuwa mwenye ujuzi;+ 23 na Berekia na Elkana watunza-malango+ kwa ajili ya Sanduku; 24 na Shebania na Yoshafati na Nethaneli na Amasai na Zekaria na Benaya na Eliezeri makuhani wakizipiga tarumbeta+ kwa sauti kubwa mbele ya sanduku la Mungu wa kweli, na Obed-edomu na Yehia watunza-malango wa Sanduku.
25 Na Daudi+ na wale wanaume wazee wa Israeli+ na wakuu+ wa maelfu wakatembea kando ili kulipandisha sanduku la agano la Yehova kutoka katika nyumba ya Obed-edomu+ kwa kushangilia.+ 26 Na ikawa kwamba wakati Mungu wa kweli alipowasaidia+ Walawi wakiwa wamelichukua sanduku la agano la Yehova, wakatoa dhabihu ng’ombe-dume saba wachanga na kondoo-dume saba.+ 27 Naye Daudi alikuwa amevaa koti lisilo na mikono la kitambaa laini, na pia Walawi wote waliochukua Sanduku na waimbaji na Kenania+ mkuu wa uchukuzi wa waimbaji;+ lakini Daudi alikuwa amevaa efodi+ ya kitani. 28 Na Waisraeli wote walikuwa wakilipandisha sanduku la agano la Yehova kwa sauti za shangwe+ na kwa kupiga baragumu+ na kwa tarumbeta+ na kwa matoazi,+ wakipiga kwa sauti kubwa vinanda na vinubi.+
29 Na ikawa kwamba wakati sanduku la agano+ la Yehova lilipokuja mpaka Jiji la Daudi, Mikali,+ binti ya Sauli, akaangalia chini kutoka dirishani, akamwona Mfalme Daudi akirukaruka na kusherehekea;+ naye akaanza kumdharau+ moyoni mwake.