1 Mambo ya Nyakati
14 Na Hiramu+ mfalme wa Tiro+ akatuma wajumbe kwa Daudi na mierezi+ na wajenzi wa kuta na wafanyakazi wa miti ili wamjengee nyumba.+ 2 Na Daudi akajua kwamba Yehova alikuwa amemfanya imara+ kuwa mfalme juu ya Israeli, kwa maana ufalme wake ulikuwa umeinuliwa sana kwa ajili ya watu wake Israeli.+
3 Na Daudi akaendelea kuchukua wake+ zaidi katika Yerusalemu, na Daudi akazaa wana na mabinti zaidi.+ 4 Na haya ndiyo majina ya watoto wake aliopata katika Yerusalemu: Shamua+ na Shobabu,+ Nathani+ na Sulemani,+ 5 na Ibhari+ na Elishua na Elpeleti,+ 6 na Noga na Nefegi+ na Yafia, 7 na Elishama+ na Beeliada na Elifeleti.+
8 Na Wafilisti wakasikia kwamba Daudi ametiwa mafuta awe mfalme juu ya Israeli wote.+ Ndipo Wafilisti wote wakaja kumtafuta Daudi.+ Daudi aliposikia habari hizo, akatoka na kwenda kupigana nao. 9 Nao Wafilisti wakaingia na kuendelea kuvamia katika nchi tambarare ya chini ya Refaimu.+ 10 Naye Daudi akaanza kumuuliza Mungu,+ akisema: “Je, nipande kwenda kupigana na Wafilisti, na je, hakika utawatia mkononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia: “Panda uende, nami hakika nitawatia mkononi mwako.” 11 Kwa hiyo Daudi akapanda kwenda Baal-perasimu+ naye akawapiga na kuwaua huko. Ndipo Daudi akasema: “Mungu wa kweli amepenya katikati ya adui zangu kupitia kwa mkono wangu kama pengo lililofanyizwa na maji.” Ndiyo sababu walipaita mahali hapo+ jina Baal-perasimu. 12 Basi wakaiacha miungu yao huko.+ Ndipo Daudi akatoa amri, nayo ikateketezwa motoni.+
13 Baadaye Wafilisti wakavamia tena katika nchi tambarare ya chini.+ 14 Ndipo Daudi akamuuliza+ tena Mungu wa kweli, na sasa Mungu wa kweli akamwambia: “Usipande kuwafuatilia. Zunguka uende, usiende moja kwa moja kuwashambulia, nawe uwajie mbele ya miti ya mibaka.+ 15 Na iwe kwamba, utakaposikia sauti ya mwendo juu ya miti ya mibaka,+ ndipo utoke, uingie katika pigano,+ kwa sababu Mungu wa kweli atakuwa ametoka kwenda mbele yako+ kuipiga kambi ya Wafilisti.” 16 Basi Daudi akafanya kama vile Mungu wa kweli alivyokuwa amemwamuru,+ nao wakaipiga kambi ya Wafilisti kutoka Gibeoni+ mpaka Gezeri.+ 17 Na sifa+ ya Daudi ikaanza kuenea katika nchi zote, na Yehova akatia hofu yake juu ya mataifa yote.+