49 Na wana wa Sauli wakawa ni Yonathani+ na Ishvi na Malki-shua,+ na majina ya binti zake wawili, jina la yule aliyezaliwa kwanza lilikuwa Merabu+ na jina la yule mdogo lilikuwa Mikali.+
11 Baadaye Sauli akatuma wajumbe+ kwa nyumba ya Daudi ili wailinde na kumuua asubuhi;+ lakini Mikali mke wake akamwambia Daudi, akisema: “Usipoiponya nafsi yako usiku wa leo, kesho utakuwa mtu aliyeuawa.”
13 Naye akasema: “Vema! Mimi nitafanya agano pamoja nawe. Ila tu kuna jambo moja ambalo ninaomba kwako, nikisema, ‘Huwezi kuuona uso wangu,+ isipokuwa kwanza umlete Mikali,+ binti ya Sauli, utakapokuja kuuona uso wangu.’”
16 Na ikawa kwamba wakati sanduku la Yehova lilipokuja ndani ya Jiji la Daudi, Mikali,+ binti ya Sauli, akaangalia chini kutoka dirishani, akamwona Mfalme Daudi akiruka na kucheza dansi huku na huku mbele za Yehova; naye akaanza kumdharau+ moyoni+ mwake.
29 Na ikawa kwamba wakati sanduku la agano+ la Yehova lilipokuja mpaka Jiji la Daudi, Mikali,+ binti ya Sauli, akaangalia chini kutoka dirishani, akamwona Mfalme Daudi akirukaruka na kusherehekea;+ naye akaanza kumdharau+ moyoni mwake.