“Chukua wewe vipande kumi; kwa maana Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Tazama, ninaurarua ufalme kutoka mkononi mwa Sulemani, nami hakika nitakupa wewe makabila kumi.+
20 Na ikawa kwamba mara tu Israeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, mara moja wakatuma watu kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya kuwa mfalme juu ya Israeli yote.+ Hakuna yeyote aliyekuwa mfuasi wa nyumba ya Daudi isipokuwa kabila la Yuda peke yake.+
2 “Kwa vile nilikusimamisha kutoka mavumbini+ ili nikufanye kiongozi juu ya watu wangu Israeli,+ lakini ukaanza kutembea katika njia ya Yeroboamu+ na hivyo kusababisha watu wangu Israeli watende dhambi kwa kunitia uchungu kwa dhambi zao,+