10 Kulikuwa na mto wa moto unaotiririka kutoka mbele zake.+ Kulikuwa na maelfu elfu walioendelea kumtumikia,+ na elfu kumi mara elfu kumi walioendelea kusimama mbele zake.+ Ile Mahakama+ ikaketi, na vitabu vikafunguliwa.
10 Angalieni msimdharau mmoja wa hawa wadogo; kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika zao+ mbinguni sikuzote huuona uso wa Baba yangu aliye mbinguni.+
11 Nami nikaona, nami nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme na wale viumbe hai na wale wazee, na hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu+ na maelfu ya maelfu,+