8 Haya ndiyo majina ya wale wanaume wenye nguvu+ waliokuwa wa Daudi: Yosheb-bashebethi+ Mtakemoni, kichwa cha wale watatu. Alikuwa akitikisa mkuki wake juu ya watu mia nane waliouawa kwa wakati mmoja.
10 Basi hawa ndio vichwa vya wale wanaume wenye nguvu+ wa Daudi, walioshikamana naye kwa nguvu katika ufalme wake pamoja na Israeli wote, kumfanya kuwa mfalme kulingana na neno la Yehova+ kuhusu Israeli.