4 Kwa maana atamgeuza mwana wako aache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine;+ na hasira ya Yehova itawaka kwelikweli juu yenu, naye hakika atakuangamiza haraka.+
8 Na kuhusu ile nyumba yake ambamo alikuwa akae, katika ule ua mwingine,+ ilikuwa mbali na ile nyumba ya Ukumbi. Ilikuwa hivyo katika muundo. Na palikuwa na nyumba kama Ukumbi huu ambayo alimjengea binti ya Farao,+ ambaye Sulemani alikuwa amemchukua.
24 Hata hivyo, binti ya Farao+ akatoka katika Jiji la Daudi+ akaenda kwenye nyumba yake mwenyewe, ambayo mfalme alikuwa amemjengea. Wakati huo ndipo Sulemani alipokijenga Kilima.+
10 Mwishowe Ezra kuhani akasimama, akawaambia: “Ninyi wenyewe mmetenda kwa kukosa uaminifu kwa vile mmewapa makao wanawake wa kigeni+ ili kuongezea hatia ya Israeli.+