40 Nawe utaishi kwa upanga wako,+ na kumtumikia ndugu yako.+ Lakini itatokea kwamba, utakapokosa utulivu, wewe hakika utavunja nira yake kutoka shingoni pako.”+
14 Naye akaweka kambi za kijeshi katika Edomu.+ Katika Edomu yote akaweka kambi za kijeshi, na Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi;+ na Yehova akaendelea kumwokoa Daudi popote alipoenda.+
9 Na mfalme wa Israeli na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu+ wakaenda, wakazidi kwenda kwa siku saba, na kukawa hakuna maji kwa ajili ya hiyo kambi na kwa ajili ya wanyama wa kufugwa waliokuwa wakifuata hatua zao.