20 Na ikawa kwamba mara tu Israeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, mara moja wakatuma watu kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya kuwa mfalme juu ya Israeli yote.+ Hakuna yeyote aliyekuwa mfuasi wa nyumba ya Daudi isipokuwa kabila la Yuda peke yake.+
11Rehoboamu alipofika Yerusalemu,+ mara moja akaikutanisha nyumba ya Yuda na Benyamini,+ wanaume bora, watu hodari wa vita,+ watu 180,000, wapigane na Israeli ili kuurudisha ufalme kwa Rehoboamu.