14 Naye akapeleka uhamishoni+ Yerusalemu yote na wakuu+ wote na wanaume mashujaa wote, wenye nguvu+—akapeleka uhamishoni watu elfu kumi—na pia kila fundi+ na mjenzi wa maboma. Hakuna yeyote aliyeachwa nyuma isipokuwa watu wa tabaka ya chini+ wa nchi.
20 Tena akawachukua mateka mpaka Babiloni wale waliobaki kutokana na upanga,+ nao wakawa watumishi wake+ na wa wanawe mpaka mamlaka ya kifalme ya Uajemi+ ilipoanza kutawala;
9 Na Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi+ akawapeleka uhamishoni kule Babiloni+ wale watu wengine walioachwa ndani ya jiji, na wale waliokimbia ili kujiunga naye, na watu wengine walioachwa.
15 Na baadhi ya watu wa hali ya chini kati ya watu na wale watu wengine walioachwa katika jiji+ na wale waliokimbia wakajiunga na mfalme wa Babiloni na wale wafanyakazi stadi wengine Nebuzaradani mkuu wa walinzi akawapeleka uhamishoni.+