2 Basi mfalme akamwambia Esta siku ya pili pia wakati wa karamu ya divai:+ “Ombi lako ni nini,+ Ee Esta, malkia? Na upewe hilo.+ Na haja yako ni nini? Hata nusu ya ufalme+—na iwe hivyo!”
12 Na mfalme akamwambia Malkia Esta:+ “Katika ngome+ ya Shushani Wayahudi wamewaua na kuwaangamiza watu mia tano pamoja na wana kumi wa Hamani. Katika wilaya nyinginezo za utawala+ wa mfalme wamefanya nini?+ Na ombi lako ni nini? Na upewe hilo.+ Na haja yako zaidi ni nini?+ Na ifanywe.”