Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 3:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Na wana wa Israeli wakaanza kumwita Yehova awape msaada.+ Ndipo Yehova akasimamisha mwokozi+ kwa ajili ya wana wa Israeli ili apate kuwaokoa, Othnieli+ mwana wa Kenasi,+ ndugu mdogo wa Kalebu.+

  • Waamuzi 4:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Na wana wa Israeli wakaanza kumlilia Yehova,+ kwa sababu Yabini alikuwa na magari 900 ya vita yenye miundu ya chuma,+ naye kwa miaka 20 akawakandamiza wana wa Israeli+ kwa ukali.

  • Waamuzi 10:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Lakini wana wa Israeli wakamwambia Yehova: “Tumetenda dhambi.+ Wewe mwenyewe ututendee kulingana na lolote lililo jema machoni pako.+ Lakini tafadhali, utukomboe tu leo hii.”+

  • 1 Samweli 7:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kwa hiyo wana wa Israeli wakamwambia Samweli: “Usikae kimya kwa ajili yetu ukose kumwomba Yehova Mungu wetu msaada,+ atukomboe kutoka mkono wa Wafilisti.”

  • Nehemia 9:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 “Lakini mara tu walipopata kupumzika, wakatenda tena mabaya mbele zako,+ nawe ukawaacha mkononi mwa adui zao, ambao waliwakanyagia chini.+ Kisha wakawa wanarudi na kukulilia wapate msaada,+ nawe ukasikia kutoka mbinguni kwenyewe+ na kuwakomboa kulingana na rehema zako nyingi, tena na tena.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki