29 Nawe kwa kweli utakuwa mtu anayepapasa-papasa katikati ya mchana, kama vile kipofu anavyopapasa-papasa gizani,+ nawe hutafanya njia zako zifanikiwe; nawe utakuwa mtu tu ambaye sikuzote hupunjwa na kunyang’anywa, pasipo mtu wa kukuokoa.+
52 Nao kwa kweli watakuzingira ndani ya malango yako yote mpaka kuta zako ndefu na zenye ngome ambazo unazitumaini zitakapoanguka katika nchi yako yote, naam, hakika watakuzingira ndani ya malango yako katika nchi yako yote, ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe.+
23 Nami nitakitia mkononi mwa wale wanaokuudhi,+ ambao wameiambia nafsi yako, ‘Inama chini ili tuvuke,’ hivi kwamba ulikuwa ukiufanya mgongo wako kama dunia, na kama barabara kwa ajili ya wale wanaovuka.”+