-
Nehemia 13:15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Katika siku hizo niliona katika Yuda watu wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya sabato+ na kuingiza marundo ya nafaka na kuyapakia+ juu ya punda,+ na pia divai, zabibu na tini+ na kila namna ya mzigo, na kuviingiza Yerusalemu siku ya sabato;+ nami nikatoa ushahidi juu yao siku waliyokuwa wakiuza vyakula.
-
-
Isaya 58:13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “Ikiwa kwa ajili ya sabato utarudisha nyuma mguu wako kuhusiana na kuyafanya mapendezi yako mwenyewe katika siku yangu takatifu,+ na kwa kweli uiite sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, inayotukuzwa,+ nawe kwa kweli uitukuze badala ya kufanya njia zako mwenyewe, badala ya kutafuta kinachokupendeza na kusema neno;
-