13 “Tieni ndani mundu,+ kwa maana mavuno yameiva.+ Njooni, teremkeni, kwa maana shinikizo la divai limejaa.+ Mitungi ya shinikizo inafurika; kwa maana ubaya wao umekuwa mwingi.+
20 Na lile shinikizo la divai likakanyagiwa nje ya jiji,+ na damu ikatoka katika lile shinikizo la divai hata kufikia juu kwenye lijamu za farasi,+ kwa umbali wa stadia elfu moja mia sita.+
15 Na upanga mrefu mkali unachomoza kutoka kinywani mwake,+ ili ayapige mataifa nao, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.+ Yeye anakanyaga pia shinikizo la divai+ ya hasira ya ghadhabu ya Mungu+ Mweza-Yote.