48 Nawe utalazimika kuwatumikia adui+ zako ambao Yehova atawatuma juu yako kwa njaa+ na kiu na uchi na uhitaji wa kila kitu; naye hakika ataweka nira ya chuma katika shingo yako mpaka atakapokuwa amekuangamiza wewe.+
27 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba mzigo wake utaondoka juu ya bega lako,+ na nira yake itaondoka juu ya shingo yako,+ na nira hakika itavunjwa+ kwa sababu ya mafuta.”
8 “Na itakuwa katika siku hiyo,” asema Yehova wa majeshi, “kwamba nitaivunja nira ya mtu kutoka shingoni mwako, na pingu zako nitazikata vipande viwili,+ na wageni hawatamtumia vibaya tena kama mtumishi.
27 Na mti wa shambani utatoa matunda+ yake, na nchi yenyewe itatoa mazao+ yake, nao kwa kweli watakuwa katika nchi yao kwa usalama.+ Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapovunja nira+ zao na kuwakomboa kutoka katika mkono wa wale waliokuwa wakiwatumia kama watumwa.+