-
Yeremia 50:29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 “Iteni wapiga-mishale juu ya Babiloni, wote wanaokanyaga upinde.+ Pigeni kambi juu yake pande zote. Wenye kuponyoka na wasiwepo.+ Mlipeni yeye kulingana na matendo yake.+ Kulingana na yote ambayo ametenda, mtendeeni vivyo hivyo.+ Kwa maana yeye ametenda kwa kimbelembele juu ya Yehova, juu ya Mtakatifu wa Israeli.+
-
-
Danieli 5:23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Bali ulijiinua juu ya Bwana wa mbingu,+ nao wakaleta mbele yako vyombo vya nyumba yake;+ na wewe pamoja na wakuu wako, masuria wako na wake zako wadogo mmekuwa mkivinywea divai. Nawe umeisifu miungu minyonge ya fedha na ya dhahabu, shaba, chuma, miti na mawe,+ ambayo haioni chochote, wala kusikia chochote, wala kujua chochote;+ lakini hukumtukuza+ Mungu ambaye pumzi yako imo mkononi mwake+ na ambaye njia zako zote ni zake.+
-