13 Kwa sababu ya ghadhabu ya Yehova yeye hatakaliwa,+ naye atakuwa mahame yenye ukiwa.+ Na yeyote anayepita kando ya Babiloni, atatazama kwa mshangao na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+
39 Kwa hiyo wakaaji wa maeneo yasiyo na maji watakaa pamoja na wanyama wenye kupiga mayowe, na mbuni watakaa ndani yake;+ na ndani yake yeye hatakaliwa tena kamwe, wala yeye hatakaa mahali popote kwa kizazi baada ya kizazi.”+
40 “Kama yalivyokuwa maangamizi ya Mungu juu ya Sodoma na Gomora+ na miji yake jirani,”+ asema Yehova, “vivyo hivyo hakuna mtu atakayekaa humo, wala mwana wa binadamu hatakaa humo akiwa mgeni.+