25 Ndipo watalazimika kusema, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano+ la Yehova Mungu wa mababu zao, ambalo alifanya pamoja nao alipowatoa katika nchi ya Misri.+
9 Nao watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova Mungu wao, aliyekuwa amewatoa mababu zao katika nchi ya Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine+ na kuiinamia na kuitumikia. Ndiyo sababu Yehova alileta juu yao msiba huu wote.’”+
22 Na utakaposema moyoni mwako,+ ‘Kwa nini mambo haya yamenipata?’+ kwa sababu ya wingi wa makosa yako marinda yako yameondolewa yasiwe kifuniko;+ visigino vyako vimetendewa kijeuri.
10 “Na itakuwa kwamba, utakapowaambia watu hawa maneno haya yote na kwa kweli wao wakuambie, ‘Kwa sababu gani Yehova amesema juu yetu msiba huu wote ulio mkubwa, nasi tuna kosa gani na dhambi gani ambayo tumemtendea Yehova Mungu wetu?’+