-
Esta 3:12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Ndipo waandishi+ wa mfalme wakaitwa katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na tatu ya mwezi huo. Basi kuandika+ kukaendelea kulingana na yote ambayo Hamani aliwaamuru maliwali wa mfalme na magavana waliokuwa juu ya wilaya mbalimbali za utawala,+ na wakuu wa vikundi mbalimbali vya watu, wa kila wilaya ya utawala, katika mtindo wao wa kuandika,+ na kila kikundi cha watu kwa lugha yao wenyewe. Hayo yaliandikwa kwa jina+ la Mfalme Ahasuero na kutiwa muhuri kwa pete+ ya mfalme.
-
-
Esta 8:9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Basi waandishi+ wa mfalme wakaitwa wakati huo katika mwezi wa tatu, yaani, mwezi wa Sivani, siku ya 23 ya mwezi huo; na Wayahudi na maliwali+ na magavana na wakuu wa wilaya za utawala ambazo zilikuwa kutoka India mpaka Ethiopia, wilaya za utawala 127,+ wakaandikiwa kulingana na yote ambayo Mordekai aliamuru. Kila wilaya ya utawala kwa mtindo wao wa kuandika+ na kila kikundi cha watu kwa lugha+ yao, na Wayahudi kwa mtindo wao wa kuandika na kwa lugha+ yao.
-